Header Ads Widget

WAUZAJI BIDHAA ZA KILIMO CHANGAMOTO KATIKA KUTOA RISITI

 



Na Fadhili Abdallah,Kigoma 


MAMLAKA  ya mapato Tanzania (TRA) Mkoani Kigoma imeeleza kuwa licha ya utoaji wa elimu ya mlipa kodi kwa jamii bado kumekuwa na changamoto ya utoaji risiti  hasa maeneo ya vijijini ambapo kumekuwa kukifanyika shughuli za kibiashara ikiwemo kilimo.



Hayo yamebainishwa na meneja wa TRA Mkoani hapa  DEOGRATIUS SHUMA katika kampeni ya TUWAJIBIKE iliyolenga kutoa elimu kwa wafanya biashara katika zoezi la ununuzi na utoaji wa risiti kwa kila bidhaa.


Shuma amesema kwa miaka ya karibuni kumekuwa na mabadiliko ya ongezeko la kutoa na kudai risiti lakini bado limekuwa halijitoshelezi kulingana na uwepo wa biashara ambazo zinatambulika na mamlaka hiyo.



Katika zoezi hilo baadhi ya wafanyabiashara waliopo katika taasisi za elimu akiwemo Starkisha Nyaga Mkuu wa shule ya msingi Shabbir ambaye  ameeleza kuwa  kumekuwa na changamoto ya upatikanaji wa risiti hasa katika manunuzi ya bidhaa za nafaka  kutoka maeneo ya vijijini.


 

Naye Martha Michael, Mhasibu kutoka  Sunset Vista Hotel ya Mjini Kigoma alisema kuwa wanapata shida kupata risiti za EFD wanapofanya manunuzi ya bidhaa za vyakula na viungo katika masoko mbalimbali ya mkoa Kigoma. 



Akizungumzia kampeni hiyo Katibu tawala msaidizi seksheni ya uchumi ofisi ya Mkuu wa  Mkoa Kigoma, Ntime Mwalyambi  alisema kuwa zoezi hilo la kuhamsisha kutoa na kudai risiti ni muhimu kwa  wafanyabiashara kuunga mkono juhudi za ukusanyaji wa mapato kwa kutumia mashine za EFD ili kuongeza pato la Taifa litakalo wezesha kuboresha mazingira ya ufanyaji biashara.


Kampeni ya TUWAJIBIKE ilizinduliwa Machi 2 mwaka huu ikiwa na malengo ya kutoa risiti halali,kudai risiti halali na kuchukua hatua kwa wauzaji wasitoa risiti halali za EFD.


Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI