Header Ads Widget

RAIS SAMIA ASHUHUDIA UTIAJI SAINI WA MIKATABA YA KUPELEKA HUDUMA YA MAWASILIANO VIJIJINI... ATOA MAAGIZO HAYA

 


Na Hamida Ramadhan Matukio Daima APP Dodoma


RAIS Samia Suluhu Hassan ameshudia Utiaji saini mikataba ya kupeleka huduma ya Mawasiliano vijijini  ambapo ameagiza Wakala wa Usambazaji Umeme vijijini (REA) kuhakikisha wanapeleka haraka umeme kwenye vitongoji ambapo Mradi wa Kusimikwa kwa Minara ya huduma za Mawasiliano umefika Mradi utakaogharimu jumla ya Fedha za kitanzania bilion 60.7 . 


Akiongea leo jijini hapa Rais Samia Amesema Mradi huo unakwenda kutoa huduma bora za Mawasiliano katika Mikoa 26 Tanzania Bara.


Amesema ipo Changamoto ya upungufu wa umeme vijijini hali inayopelekea wananchi kushindwa kupata huduma hiyo ya Mawasiliano Hali inayopelekea kutokuwa na Maendeleo yao na. Taifa kwa ujumla.


Pia amezitaka halmashauri na Taasisi zote zinazohusika na Utiaji wa vibali kuhakikisha wanatoa vibali hivyo haraka ndani ya wiki moja na sio miezi kwa miezi. 


" Najua kuna watu wazito Kutoa vibali hivyo  kwa wale wenye makoti mazito sasa wavue makoti yao na waweze Kutoa vibali kwa sheria na taratibu zilizowekwa, "Amesema


Aidha Tarula na Mfuko wa Mawasiliano kwa UCSAF kukaa Pamoja ,kuongea na kuandaa barabara ni wapi mkongo wa Taifa wa Mawasiliano wapi utapita.


MKURUGENZI WA USCAF 


Akizungumza katika hafla hiyo Mtendaji Mkuu wa UCSAF Justina Mashiba amesema katika kuhakikisha wanafikisha huduma ya mawasiliano vijijini wanaenda kujenga minara 758 katika kata 713.


Amesema katika minara hiyo Shirika la Mawasiliano Tanzania (TTCL) walishinda zabuni katika kata   104 na watajenga minara 104, Vodacom  Tanzania  amelishinda kata 190 watajenga  minara 190,  Airtel Tanzania walishinda  kata  161 na watajenga  minara 168 , Tigo walishinda zabuni katika   kata 244 na  watajenga minara 262 na  Haloteli walishinda zabuni katika kata   34 na watajenga minara 34.


Aidha , amesema pia katika mkataba huo wanaenda kuongea nguvu katika minara 304 ambayo ilikuwa inatoa huduma ya 2G sasa itaanza kutoa huduma kwa 3G na maeneo mengine 4G.


“Lengo kubwa la kuanzisha UCSAF  ni kupeleka mawasiliano maeneo ya vijijini   na kuhakikisha watanzania wanapata huduma ya mawasiliano bila vikwazo ambapo katika kuhakikisha hilo hadi sasa tumeshajenga minara nchi nzima .


Ameongeza kuwa :”USCAF Imepeleka vifaa vya TEHAMA katika shule za umma ambapo hadi sasa tumepeleka katika shule 4750.pia tunaendelea na mradi wa tiba mtandao lengo ni kuhakikisha watanzania wanapata huduma bila kwenda Hospitali.


Justina amefafanua kuwa lengo la mfuko ni kuhakikisha wanafikisha mawasiliano mipakani na katika mbuga za wanyama.


Naye Waziri wa Habari ,Mawasiliano na Teknolojia ya Habari Nape Nnauye Amesema Jumla ya minara 758 inakwenda kuweka katika vijiji ambapo watanzania Milioni 8.5 wanakwenda kunufaika na Huduma hiyo ya mawasiliano.


MKUU WA MKOA


Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Rosemary Senyamule alisema  minara  hiyo ya mawasiliano itafanya Tanzania ifunguke Kimataifa.


Amesema mkoa wa Dodoma una maeneo mengi ambayo bado mawasiliano hayafiki  hivyo kupitia minara 758 ambayo  itajengwa na mkoa wa Dodoma itanufaika.


“Kupitia mradi wa mawasiliao kwa wote mkoa wa Dodoma unanufaika na minara 77 katika kata 56 na vijiji 202. Minara hiyo ilitumia zaidi ya sh.bilioni 11 kujegwa haya ni mafanikio makubwa na kufungua nchi kwa kiwango cha hali ya juu


"Sisi mkoa wa Dodoma tunakupongeza kwa kazi hii kuwa unayoifanya na sisi tulikuwa tunaandaa program ya kufuatilia minara  hata tukiwa ofisini hivyo tunaamini kuimarika kwa huduma hii kutaifungua kila sekta..


CHONGOLO


Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi (CCM)  ameahidi kutoa kompyuta 50 kwa serikali lengo  kuongeza chachu ya mafunzo kwa kutumia TEHAMA  shuleni.


Chongolo amesema matumizi ya teknolojia yanaweza kuturahisihsia  mambo na kuongeza chachu ya maendeleo.


“Kwa tukio hili muhimu  la utiaji saini ujenzi wa minara ya mawasiliao kwa niaba ya CCM tunaipongeza serikali  kwa kuchukua uamuzi wa msingi ambao unaenda kutekeleza ilani ya uchaguzi ya 2020/2025 kwa kiwango kikubwa.


Ameongeza kuwa :”Kwa niaba ya CCM  tumeamua kuweka ndoano ilituvune kirahisi  na kwa kuanzia CCM itatoa kompyuta 50  ili angalau kuweka chachu ya msukumo wa utekelezaji wa ilani katika teknolojia  na mawasiliano katika shule zetu nchini.



Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI