Header Ads Widget

WAFUGAJI TARAFA YA ISIMANI KUSHIRIKIANA NA POLISI KUFICHUA WEZI WA MIFUGO

 


WANANCHI wa  tarafa ya  Ismani wilaya  ya  Iringa  mkoani  Iringa  wamesema  watashirikiana na  jeshi la  polisi wilaya ya  Iringa  kuwafichua   watu  wanaojihusisha na  wizi  wa  mifugo  ili  sheria   ichukue  mkondo  wake .

Wakizungumza  leo  mbele ya  mkuu wa  polisi  wilaya ya Iringa (OCD) Bernad Samala  wananchi hao  walisema  kuwa  vimeanza  kuibuka  vitendo  vya  wizi  wa  mifugo  katika  tarafa  yao na  wahusika  hawatoki  mbali na  tarafa   hiyo  na  ni watu  ambao  wanatoka  ndani ya  tarafa   hiyo na baadhi yao  majina  yao  wanayo.


Hivyo  waliomba   kupitia  vikao  vyao  vya  vijiji ,kata na tarafa   wataendelea  kuwafichua   wezi  hao  kupitia  vikao  hivyo ambavyo pia wamekwisha  unda kanda  maalum   ya  kuthibiti  wizi wa  mifugo  ambayo  itajumuisha kata  sita  katika  tarafa  hiyo ya Isimani .

Mwenyekiti wa  wafugaji kanda ya  Isimani Baraka  Sosopi  alisema  kuwa   kupitia mkakatii  wao  wa  kuunda kanda maalumu  ya  kuthibiti  wizi wa  mifugo  wanaimani   kubwa   watafanikisha vita   dhidi ya  vitendo vya  wizi  wa  mifugo .

Kwani  walisema  kuwa  wezi hao wa  mifugo  wamekuwa  wakijigamba   wazi wazi  kuwa  hakuna  wa  kuwafanya  lolote kwani enzi  za  utawala  wa Magufuli  waliishi  kwa  hofu  kutokana na kubanwa ila  sasa wanadai  wapo  huru jambo  ambalo limekuwa  likitishia  usalama  wa mifugo yao .

Akizungumza  mara  baada ya  kikao  hicho mkuu  wa  polisi  wilaya ya  Iringa (OCD) Samali  alisema  kuwa   wao kama  jeshi la  polisi  wanataka   kuona  wafugaji na  wananchi  wa  wilaya ya Iringa  wanaishi  kwa uhuru  pasipo  kuwepo  vitendo  vya  vyovyote  vinavyotishia  usalama  wa  rai ana mali  zao .

Mkuu   huyo  wa  polisi  alisema kuwa kupitia  kikao  hicho jeshi la  polisi linaamini kuwa vitendo  vya wizi  wa mifugo na mali  za wananchi  katika  eneo hilo vitakwenda  kwisha .

Hivyo  aliwataka  wananchi  wasiogope  kuwataja kwa  siri  wale  wote  wanaojihusisha na  vitendo  vya uhalifu   ili  jeshi la  polisi  liweze  kuwakamata kwa  uchunguzi  zaidi kabla ya  kufikishwa mbele ya  vyombo  vya sheria.




Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI