Header Ads Widget

VIJANA TOKA MAZINGIRA MAGUMU MUFINDI WAANZA KUPEWA ELIMU YA SAIKOLOJIA

MRADI wa Youth Angency Mufindi (YAM) umeanza utoaji wa  elimu ya Saikolojia Kwa vijana chini ya miaka 25 wanaotoka Katika mazingira Magumu kata tatu za wilaya ya Mufindi   kuwawezesha  kukabiliana na tatizo la msongo wa mawazo na Sonona

Mafunzo hayo ya siku 10 yameanza kutolewa jana Katika Ukumbi wa Yatima Igoda wilayani Mufindi Kwa kuunganisha vijana 100 toka vijiji 16 vya Kata ya Ihanu ,Mdabulo na Luhunga .

Akizungumza na vijana hao wakati wa Ufunguzi wa mafunzo hayo ,Mwenyekiti wa chama cha Watoa huduma za kisaikolojia Tanzania Dr Heriel Mfangavo alisema  mafunzo hayo  ni fursa kubwa Kwa vijana hao Kuelekea kujitambua na Kuondokana na mawazo mgando ya kutopiga hatua ya kimaendeleo na kuwa na mawazo ya kusonga mbele .


Alisema kuwa  vijana hao ni wadogo kama hahatapatiwa tiba ya saikolojia mapema tatizo hilo wanakuwa nao na ukubwani wanaweza kufanya majanga makubwa yakiwemo ya mauwaji au kujiua .


Kwani alisema mfano mabinti waliopata mimba utotoni Kwa kubakwa ama kurubuniwa Hali hiyo huwa haifutiki kirahisi kwenye akili zao hivyo lazima elimu ya saikolojia iwapitie mapema ili wasiendelee kuteseka ama kutesa watoto .


Mbali ya mabinti pia alisema vijana walionyanyasika Kwenye familia Kwa kutelekezwa na baba mzazi wakiwa wadogo ama kupokonywa mali huwa wanakuwa na visasi hadi ukubwani.


Pia alisema kundi jingine linalohitaji msaada wa kisaikolojia ni kundi la watu wenye ulemavu ambao baadhi yao wanaishi na msongo wa mawazo na Sonona kutokana na vile walivyo .



Hivyo alisema wanasihi watakaofanya kazi  katika mradi wa Youth Agency Mufindi (YAM) wilaya ya  Mufindi  mkoani Iringa wametakiwa kubaini changamoto zinazosababisha tatizo la msongo wa mawazo Kwa jamii ya watu wenye ulemavu na kuitafutia ufumbuzi

Alisema kutokana na ukubwa wa tatizo  kwa vijana hao na  watu  wenye  ulamavu  mafunzo hayo yatakuwa na faida  kubwa kwao na  kuondokana na utegemezi .

Alisema  kuwa  mradi  huo  wa  YAM   ni mkombozi mkubwa  kwa jamii ya  wana Mufindi  hasa maeneo ambayo yanazungukwa na  mradi huo  kwani  utasaidia jamii   yenye  uhitaji  kuishi kwa  furaha  zaidi  .

Hivyo  alisema  suala la ulemavu  linapelekea   watu  wengi kuishi  kwa  misongo ya mawazo na hata  kupata  matatizo mengine ya  kiakili .

Dkt  Mfungamo  alisema  baadhi ya mambo  yamekuwa  chanzo  cha jamii  kukutwa na msongo  wa  mawazo kama  kukataliwa  ,kutengwa na  unanyapaa wa  kimahusiano .


Pia  alisema  hali  duni ya  kiuchumi inapelekea  watu  kupata  msongo wa mawazo  hivyo  kupitia mafunzo hayo  yanayotolewa  ni wazi  jamii  itakwenda  kupunguza tatizo la msongo wa mawazo na hata  kuweze kufanya  shughuli  kifanisi zaidi.

Kwa upande wao vijana  wanaotoka Katika familia duni waliokatisha masomo kutokana na changamoto mbali mbali ikiwemo ya mimba Kwa mabinti wamepongeza mradi wa Youth Agency Mufindi (YAM) kwa kuwafikia kuwapa mafunzo ya Afya ya akili na msaada wa kisaikolojia .


Washiriki wa mafunzo hayo Agnes Kihongole mkazi wa Kanig'ombe  akizungumza Kwa niaba ya wenzake alisema walifikia hatua ya kukata tamaa ya maisha baada ya kukosa fursa za elimu .


Kwani alisema Kwa upande wake hakubahatika kuendelea na Masomo ya Sekondari kutokana na wazazi wake kukosa ada.

Hivyo alisema kupitia mafunzo hayo ambayo ni mwanzo kwao kujitambua na pindi watakapojitambua ni rahisi kwao kufanya shughuli za kiuchumi.

"Tunaamini kupitia mafunzo haya tumepata ukombozi Katika maisha yetu na familia tunazotoka maana bila kujitambua ni vigumu kubaini nini Cha kufanya"

Pia alisema matarajio yake na wenzake ni  kupewa nguvu ya uwezeshwaji ili kutimiza ndoto yao hiyo .

Akizungumza Kwa niaba ya Meneja mradi wa Yam Danford Mkumbo ambae ni afisa mradi huo  alisema mradi huo ni WA Miaka minne unatekelezwa na Halmashauri ya Mufindi Kwa kushirikiana na mradi wa Foxes Community and wildlife conservation(FCWC) kupitia mradi wa YAM chini ya  ufadhili wa Serikali ya watu Finland utakelekelezwa kwenye  utanufaisha  vijana na  watoto  wanaotoka  katika  familia duni zaidi ya   vijana 770  atika  vijiji 16.

Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI