Header Ads Widget

SERIKALI YATOA MAAGIZO KWA WANAOFANYA UVUVI KWENYE VYANZO VYA MAJI

 


Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais Khamis Hamza Khamis amewataka  wawekezaji wanaofanya shughuli za uzalishaji kwenye vyanzo vya maji kuhakikisha  wanatii sheria kwa kutunza vyanzo vya maji.


 Khamis ametoa agizo hilo alipotembelea kampuni ya Tangreen Agriculture Limited kinachojishughulisha na uvuvi wa samaki kwa njia ya vizimba kilichopo Kijiji cha Kigangama Kata ya Kitongosima Wilaya ya Magu Mkoani Mwanza akiwa kwenye ziara ya kikazi mkoani Mwanza.



 Katika hatua nyingine naibu waziri Khamis amewataka wawelezaji wote nchini wanaojenga viwanda ambavyo vinatumia moto kuyeyusha malighafi watumie teknolojia mpya zinazothibiti kelele na moshi ili kutowapa athari wananchi.


 Agizo hilo pia amelitoa jijini Mwanza na alipotembelea ujenzi wa kiwanda  cha Ziwa Steel And Wire Product kitakachotengeneza  nondo na mabati kilichopo Kata ya Nyanguge Tarafa ya Kahangala Wilaya ya Magu Mkoani Mwanza.


Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI