Header Ads Widget

UWT MOSHI MJINI WAANDAA BONANZA. GEKUL ATOA NENO....

 








Na Gift Mongi,MATUKIO DAIMA APP,Moshi

 Naibu waziri wa utamaduni sanaa na michezo Pauline Gekul amezitaka halmashauri zote  katika mkoa wa kKilimanjaro kuhakikisha zinatenga fedha kwaajili ya uendeshaji wa michezo ili  kuhakikisha viwanja pamoja na vifaa vya michezo vinapatikana. 


Aidha amezitaka serikali za mitaa kuhakikisha wanakuwa  na maeneo kwa ajili ya michezo ili kukuza vipaji vya watoto pamoja na vijana pamoja na kuimarisha afya kupitia michezo.


Gekul ametoa agizo hilo  katika bonanza  la michezo lililoandaliwa na shirika la kuwezesha wanawake(Florida  women empowerment) kushirikiana na umoja wa wanawake Tanzania wilaya ya Moshi Mjini lengo likiwa ni kuunga mkono juhudi za Rais Dkt Samia Suluhu Hassan katika kuhamasisha michezo nchini.


Bonanza hilo lilihusisha michezo mbalimbali ikiwemo mpira wa miguu, mpira wa pete ,kuvuta kamba,, kukimbia na magunia kufukuza kuku,kukimbia na yai kwenye kijiko, mdako, mchezo wa kuruka kamba huku washindi wakikabidhiwa zawadi mbalimbali  na kusindikizwa na  burudani kutoka kwa wasanii wa  mkoani hapa.


Waziri Gekul amesema ili kuendelea kuimarisha sekta ya michezo, viongozi kuanzia serikali za mitaa wanapaswa kuhakikisha wanatenga maeneo ya michezo,  kuyalinda yasivamiwe na kuyaendeleza ili kuwasaidia wananchi na kukuza vipaji vya watoto pamoja vijana.


 "Viongozi wa halmashauri mnapaswa kuhakikisha mnatenga fedha kwenye bajeti zenu kwaajili ya kuendesha  michezo, suala la michezo ni la kila mmoja wetu, na jamii yote inapaswa kushiriki katika michezo, hakikisheni kwenye mitaa yenu mnakua na viwanja vya michezo, mnavitenga, mnavilinda  na kama vipo hakikisheni  mnaviendeleza" amesema Gekul na kuongeza 


"Tunapoendesha michezo tujue tunajenga afya, mahusiano, undugu, tunaibua vipaji  lakini pia tuajenga ajira, lakini kwa sasa hali ilivyo nchini kama sio kombe la mwenyekiti wa mtaa ni kombe la diwani au la mbunge, niwaombe viongozi wetu tengeni fedha kwaajili ya kuendesha michezo"amesema


Akizungumza katika bonanza hilo, Katibu wa chama cha mapinduzi wilaya ya moshi Mjini Ibrahimu Mjanaheri ameitaka serikali kuendelea kuwajengea uwezo vijana wenye vipaji na makundi ya sanaa  ili waweze kufikisha jumbe zao kwenye jamii.


"Tumeona kijana ameimba wimbo mzuri ambao wote umetuamsha hisia, na kutukumbusha umuhimu wa mama, kijana huyu anakipaji kizuri anachohitaji ni  muda wa hewani kwenye vyombo vya habari ili aweze kutambulika,wapo wengine wenye uwezo wanachohitaji ni kuongezewa uwezo  wa nyenzo pamoja na ujuzi "amesema Mjanaheri..


Kwa upande wake mwenyekiti wa UWT wilaya ya moshi mjini Theresia Komba amesema zipo programu mbalimbali za kimichezo  zilizoandaliwa kwaajili ya wanawake na wasichana ambazo zimelenga kuwainua kiuchumi na kuwawezesha  kukabiliana na aina yoyote ya dhuluma, manyanyaso, ukatili na ubaguzi.

Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI