Hospitali
ya Rufaa mkoa wa Iringa ikishirikiana na waandishi wahabari mkoani hamo,
wameanzisha kampeni ya utoaji elimu kwa wananchi juu ya uchangiaji damu ili kuepukana
na uhaba wa damu salama unayo ikabili hospitali hiyo kwa hivi sasa.
Akielezea
kampeni hiyo mganga mfawidhi wa hospital ya rufaa mkoa wa Iringa Daktari,
Alfred Laison Mwakalebela amesema kampeni hiyo
itakwenda sambamba na uzinduzi wa uchangiaji damu tarehe 1,1,2023 ikiwa
ni siku ya kwanza ya mwaka mpya, uku zoezi
hili likiwa na kauli mbiu ya inayosema “zawadi ya mwaka mpya kwa wananchi wa Iringa katika kuboresha afya
watu wasiishiwe na damu na wasipate madhara kutokana na upungufu wa damu”.
Dkt,
Mwakalebela amesema mkoa wa Iringa kwa ujumla unatumia chupa za damu salama mia
sita kwa mwezi uku tegemeo kubwa likiwa ni wanafunzi wa shule za sekondari na
kipindi shule zikifungwa mkoa huo unakabiliwa na upungufu wa damu salama.
Amewataka viongozi
mbalimbali katika ngazi zote kuwahamasisha
wa wananchi wao kuwa na tabia ya kujitolea damu ili kuweza kuokoa Maisha ya
watanzania wengine, “Nipende kuwahamasisha wananchi wa mkoa wa Iringa, taasisi
mbalimbali zihamasishe watumishi wake, viongozi wa bodaboda kwa pamoja waungane
pamoja na viongozi wa dini kuwahamasisha waumini wao kila wanapokuwa ibadani
ili kuwezesha tabia ya uchangiaji damu”.
Kwa upande
wake, muuguzi mkuu mkoa wa Iringa Mosses Kawete, amesema mkoa huo umejipanga
vizuri kwa kushirikiana na wakurugenzi wa halmashauri zote za mkoa huo kwa kutoa
muongozo ambao utapeleke zoezi hilo kuwa endelevu ili kuondokana na upungufu
unatokea mara kwa mara katika mkoa huo uku akiitaja Halmashauri ya mji wa
Mafinga kuwa kinara katika uchangiaji wa damu katika mkoa wa Iringa.
Naye mwakilishi
wa wanahabari mkoa wa Iringa, Silvanus Kigomba ameelezea sababu zilizopelekea kuunga
na hospitali ya rufaa ya Iringa katika kuanda kampeni hiyo ya kuhamasisha
uchangiaji damu kwa wananchi wa ili kuweza kuwaokoa wagonjwa wanaofika katika
hospitali hiyo wakihitaji damu, pamoja na kuelezea utaratibu wa kutembela taasisi
mbalimbali pamoja nanyumba za ibada ili kuwahamasisha waumini kujitokeza katika
zoezi hilo ambalo uzinduzi wake ni tarehe 1,1,2023.
“Tumeanda
utaratibu mbalimbali wa kuwatembelea wananchi ikiwemo kuandika barua ambazo
zipelekwa katika nyumba zote za ibada katika ili kila muumini na dini yake
apate taarifa hii na kuweza kujitokeza kwani zoezi hili ni endelevu hivyo tutakuwa
tunakumbushana mara kwa mara”
0 Comments