NA AMINA SAID,MATUKIO DAIMAAPP,TANGA
Mwenyekiti mpya wa Chama cha Mapinduzi Mkoa wa Tanga Rajabu Abdarahman Abdalah amesema kuwa upinzani kwa mkoa wa Tanga umefikia mwisho
Hayo aliyasema katika mkutano wa hadhara wa Mbunge wa jimbo Pangani na Waziri wa maji Juma Aweso, iliyofanyika wilayani Pangani kwa ajili ya kusherekea ushindi wa kushika wadhifa kuwa Mwenyekiti kwa kura 1340 kati ya kura 1385.
Aidha mwenyekiti Rajabu alisema kuwa lengo lake kubwa la kugombea nafasi hiyo ni kushika dola ili aweze kusimamia ili kuweza kumsaidia rais Samia suluhu Hassan kuhakiksha nchi inasonga mbele.
Alisema kuwa katika mkoa wa Tanga atahakikisha wapinzani wanasambaratika ili Chama cha Mapinduzi Mkoa iweze kushika dola ili ifikapo 2025 kusiwe na upinzani katika uchaguzi mkuu na mkoa wa Tanga uongoze katika uchaguzi na kumuunga mkono Mh.Samia suluhu Hassan kwa maslahi mapana ya wanatanga.
Kwa upande wake Mnek ambaye Mohamedi Ratico alitoa rai kwa wabunge wote wa mkoa wa Tanga wawe na desturi yankufanya mikutano ya hadhara kwalengo la kujua changamoto za wananchi na kuweza kuzitatua .
0 Comments