Header Ads Widget

MWAKA 2023 UNA DALILI ZA MAFANIKIO MAKUBWA - ASKOFU Dkt GAVILE

 ASKOFU  wa kanisa la  kiinjili la  Kilutheri  Tanzania (KKKT) dayosisi ya  Iringa  Dkt Blaston Gavile amesema  kuwa  mwaka  ujao 2023  ni mwaka  wenye dalili  za  mafaniko  mengi ya  mwilini na rohoni  hivyo ataka  angalizo  kubwa  kuwepo ikiwa ni pamoja na  kuweka akiba ya mafanikio yatakayopatikana.


"Kama  wachungaji  naweka angalizo ,mwaka ukiwa na neema wengi  tunajisahau na  kuona ni  haki yetu  kupata  mema  bado nasisitiza tuweke akiba tutunze sisi kwa  sisio  tuombeane uzima kama familia" 


Askofu  Dkt  Gavile  aliyasema hayo  juzi wakati akitoa  salamu  za  Krismasi  katika ibada iliyofanyika  usharika  wa Kanisa kuu Iringa  ,  kuwa  mbali ya mwaka ujao  kuwa ni mwaka  wa  neema  bado  wananchi  wanapaswa  kutumia  vizuri  mvua za  kwanza  kuwa ni mvua ya  kupandia mazao badala ya  kuzitumia kuandaa mashamba .



Pia  alitaka kila  mmoja  kuweka akiba ya chakula  atakachokipata  ili  kuwa na akiba  endelevu  ya  chakula kuwa  iwapo  akiba ya  chakula  itatunzwa  vizuri  si rahisi pale  mvua  zinapochelewa  kunyesha watu  kuwa na  hofu ya  njaa kwani tayari  kila  mmoja  anakuwa na akiba  yake  mwenyewe ya  chakula ndani .


Dkt Gavile  alisema maandalizi  mema ya  familia  yanapaswa  kwenda  sanjari na maandalizi  mazuri ya kuwaandaa watoto  vizuri  kwa  ajili ya  shule  kwani  ili  wasome  vizuri  yanahitajika  maandalizi  mazuri ya  wazazi  ili  watoto   wasikwame  kwenda shule  kutokana na  sababu  zozote  zile .

Hata  hivyo  aliwataka  watanzania  kuendelea kuomba  kwa  ajili ya Taifa  pamoja na  kumuombea Rais wa  Jamhuri ya  Muungano  wa Tanzania  Dkt  Samia Suluhu  Hassan  pamoja na watenda  kazi wenzake  ili  nchi iendelee kuwa na amani na mshikamano .

Katika  hatua  nyingine  askofu   huyo  ameitaka  jamii hasa ya  mkoa wa  Iringa  kuendelea  kuomba na kukemea hali ya  vitendo viovu   vya  ukatili  wa  kijinsia  kwani  vitendo  hivyo  kwa  sasa ndani ya  mkoa  huo  vimeshika kasi  hivyo  lazima  kuchukua  tahadhali  ikiwa ni  pamoja na  kutoa taarifa  kwenye  vyombo  vuya ulinzi  na usalama  pindi  vitendo  hivyo  vinapotokea katika maeneo  yetu.

Aidha  askofu  Dkt  Gavile  alisema huu ni mwaka wa pekee ambao tunaadhimisha Krismas, tukiwa na baraka ya hali ya mvua, lakini tunasheherekea sikukuu hii mwaka huu bila KOVID 19 ni wema wa MUNGU tu, Mwaka 2022 umekuwa na mambo mengi sana yaliyo ya baraka, Mungu ametupitisha na kutuvusha katika mambo katika mambo mengi na ratiba nyingi, katika yote Mungu ametupigania, kuna wakati tumepita katika moto lakini hakutuacha tuangamie. Wapo kati yetu waliugua sana na kuuguza sana, hata hivyo wema wa Mungu umetuzunguka. Kweli hata sasa Bwana ametusaidia(Ebenezer).

Kwangu mwaka 2022 umekuwa ni mwaka wa kukumbuka sana hasa matukio mengi ya kanisa ndani ya Iringa na nje ya Dayosisi yetu ya Iringa, ikiwemo Mkutano wa wachungaji wote wa KKKT Tanzania nzima uliofanyika Dodoma, Mkutano wa wachungaji wa Dayosisi ya Iringauliofanyika Chuo Kikuu cha Iringa, Mkutano wa kurugenzi ya wanawake, malezi ya familia na watoto uliofanyika Arusha, Mkutano wa wachungaji watheolojia wanawake uliofanyika Njombe, uzinduzi wa Dayosisi ya Magharibi Kigoma, Mkutano wa LMC Mwanza, Mkutano Mkuu wa Dayosisi wenye wajumbe wapatao 700 ambao ulikuwa na uchaguzi wa saidizi wa askofu, na kwa pamoja Mkutano ulimchagua Mchungaji Askali Mgeyekwa kuwa Msaidizi wa Askofu kwa kipindi cha miaka 6 kuanzia 2022-2028. piamkutano uliwachagua wakuu wa majimbo na Idara.


Pia kumekuwa na zoezi la kuwaingiza kazini wakuu wa majimbo pamoja na wajumbe wa Halmashauri kuu, wakuu wa idara, vituo, vitengo na Taasisi, alisema Askofu Dkt Gavile.

Kwa upande wa usharika askofu Dkt Gavile amesema kuna ujenzi mkubwa wa makanisa ya kisasa unaendelea, nyumba za kisasa za watumishi, vitega uchumi mbalimbali vya sharika, sharika kumi mpya zitazaliwa 2023 na pia kuna ongezeko kubwa la wakristo.

Kwa kumalizia Askofu dkt gavile amesema mwaka 2022 ni mwaka ambao tulimwahidi Mungu kufanya mambo kadha wa kadha, mengine hata sasa hayajafanyika. Mwaka huu unapokwisha tumwungamie Mungu kwa mengi tuliyoshindwa na hata kutimiza wajibu wetu, Tumalize kwa toba, Lakini pia tuna mambo mengi tumemkosea Mungu. Kinachofurahisha Mungu ni moyo wa Toba, unyenyekevu na moyo wa Shukrani.






Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



BBC NEWS