Header Ads Widget

MASIKINI DIAMOND PLATNUMZ TUENDELEE KUMUOMBEA


 Mashabiki wa msanii namba moja wa muda wote ukanda wa Afrika Mashariki katika kitengo cha muziki wa Bongo Fleva, Diamond Platnumz wamejawa na wasiwasi baada ya msanii wao pendwa kupakia video kwenye instastory yake akiwa amelazwa hospitalini.

Diamond alipakia kipande hicho cha video kwenye Instagram yake na alionekana kuwa katika kitanda cha hospitali akiwa ametundikwa drip ya maji huku akifuatisha kwa maandishi ya mashaka kuwa huu ndio msimu wa krismasi mbaya sana katika maisha yake kwani amelazimika kusalia katika kitanda cha hospitali sikukuu ya Krismasi.

Katika vido hiyo, Diamond Platnumz alionekana mwenye maumivu makali huku akipata taabu sana kujipendua na kujisogeza. Kando ya kitanda cha hospitali paliponekana mama mmoja anayekisiwa kuwa mama Dangote akiwa ameweka mikono yake kwa nyuma kwa wasiwasi mno akimtizama mwanawe jinsi anajigaragaza kitandani kwa uchungu na maumivu.

Video hiyo pia inaendelea wakionekana matabibu na wauguzi wakijitahidi kwa hali na mali kumwekea drip za maji kwenye mkono wake.

Mashabiki wake walifurika mitandaoni na kumtakia kheri njema na nafuu ya haraka huku wengine wakizusha kuwa huenda ni moja ya kiki zake za kila mara ambazo wamezoea kutoka kwake.

Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



BBC NEWS