Header Ads Widget

TRA MTWARA WASHIRIKI USAFI

 




Baadhi ya watumishi wa  Mamlaka ya mapato Tanzania TRA Mkoa wa Mtwara wakishirikiana na wananchi na taasisi zingine wamefanya usafi katika

maeneo mbalimbali kata ya Chikongola Manispaa ya Mtwara Mikindani ili

kuweza kuhamasisha ufanyaji wa usafi kwa wakazi wa maeneo hayo.


Akizungumza kwenye maadhimisho ya siku ya shukrani kwa mlipakodi

Kaimu Meneja wa TRA Mkoa wa Mtwara Elirehema Kimambo alisema kuwa

wamefanya usafi ili kweza kuhamasisha jamii kuwa na utaratibu wa

kulipa kodi.


“Sisi ni sehemu ya jamii siku hii ni muhimu kwetu ili kujenga uhusiano

wa karibu kati yetu na wafayabishara na kuonyesha kwamba zoezi la

kukusanyaji wa kodi ni zoezi letu ni kwaajili ya kupendezesha mji wetu

wa Mtwara” alisema Kimambo


Mkuu wa Wilaya ya Mtwara Dunstan Kyobya aliagiza zoezi hilo kufanyika

kila jumamosi.


“Zoezi lifanyike kila jumamos nitambue kazi nzuri inayofanywa na TRA

ambapo wanarudisha faida wanayoipata kupitia ulipaji kodi tunaoufanya

naamini maeneo yaote ya masoko yatawekwa dustben ili mtu aweze kutupa”


Nataka hili zoezi la usafi liwe endelevu kwa kila kata elimu ya usafi

itolewe kwa wananchi vizimba vitolewe uchafu ili kutoa nafasi ya

kuhifahdi uchafu mwinginen kwa wakati” alisema Kyobya


Kwa upande wake mkurugenzi wa Manispaa ya Mtwara Mikindani Kanal

Emmanuel Mwaigobeko alisema kuwa wataendela kufanya usafi kila

jumamosi ili kuweka mji huo katika hali ya usafi.


“Hili zoezi ni zuri na litakuwa endelevu tunaamini kuwa tutapanga kila

jumamosi tuwe tunafanyausafi ili kuifanya jamii yetu kuwa katika

mwonekano mzuri kwa kuhama kata hadi kata” alisema Kanal Mwaigobeko


Nae Diwani wa kata ya chikongola mussa Namtema alisema kuwa suala la

usafi limekuwa ni desturi kwa ofisi yake kuhamasisha wananchi hivyo

kupitia zoezi hilo wananachi wengi watajifunza.


“Tulikuw atunafanya usafi kila baada ya wiki mbili na zoezi endelevu

tumeona hamasa kubwa itakuwa aibu taasisi iwe na uchafu mbele yake

chukueni hatua  imeonyeshwa wananchi” alisema Namtema


MWISHO

Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI