Na Eliza Ntambala
Mkuu wa mkoa wa Rukwa Queen Sendiga amefanya ukaguzi wa Miradi mbalimbali ya Maendeleo Wilayani Nkasi unaendelea,Ujenzi kituo Cha Afya Kasu,Jengo la Dharura Hospitali ya Wilaya,kituo cha Afya Kabwe na shughuli mbalimbali Bandari ya Kabwe ambapo ameagiza utekelezaji wa shughuli muhimu kuweza kukamilika kwa wakati ili kuwezesha utoaji wa huduma kwa wakati.
Akiwa Katika mkutano wa Hadhara na wananchi kata ya Kabwe, moja ya malalamiko ya wananchi wamesema wanashangaa kuona watendaji kata wakihamishwa huku wakidaiwa kutotimiza wajibu wao na kusababisha Miradi kuwa na harufu ya ubadhirifu hivyo nimeagiza Wakurugenzi kuhakikisha watendaji wote Katika Mkoa wa Rukwa ambao walihamishwa baada ya kushindwa kutimiza majukumu yao na kupelekwa sehemu nyingine warudishwe wamalizane na changamoto walizozianzisha na hatua za kinidhamu zichukuliwe kwa yeyote aliesababisha uzembe wa kuzorotesha ama kuhujumu miradi.
0 Comments