Header Ads Widget

PROFESA MAGHEMBE ATAKA ELIMU YA MSINGI IWE MIAKA SITA.

 



ALIYEWAHI kuwa Waziri wa Elimu Profesa Jumanne  Magembe ameunga mkono kupunguza miaka ya elimu ya Msingi kutoka miaka saba hadi sita.


Aidha ametaka kufanyika maboresho ya elimu ya awali ili iendane na maboresho ya Elimu ya Msingi.


Maghembe aliyasema hayo  Wilayani Mwanga Mkoani Kilimanjaro alipozungumza na waandishi wa habari kuwa ili kuendana na hali halisi ya sasa haipaswi wanafunzi kusoma muda mrefu. 


Maghembe ambaye pia aliwahi kuwa Mbunge wa Jimbo la Mwanga alisema kuwa elimu ya sasa inafuata misingi ya kikoloni ambapo mwanzo waliwasomesha watoto muda mrefu.


Alisema waliweka miaka mingi wawe wakubwa ili wakimaliza wawe walimu na makarani. 


Alisema kuwa ili kuendana na miaka sita kuna haja ya kuhakikisha elimu ya awali inaboreshwa.

Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI