Na,Esther Macha,Matukio daima Media,Mbeya
TAASISI ya kuzuia na kupambana na Rushwa mkoani Mbeya imesema kuwa inachunguza wasimamizi wawili wa Sensa ya watu na Makazi ambao wanadaiwa kuhusika kupokea Rushwa ya sh.20,0000 kwa kila mmoja ili wawapitishe makarani kwenye usaili ili waweze kushiriki zoezi la sensa ambalo limeanza Agosti 23 mwaka huu .
Akizungumza na waandishi wa habari leo Mkuu wa Takukuru mkoa wa Mbeya ,Maghela Ndimbo amesema hayo wakati akitoa taarifa ya miezi mitatu ambayo ni April mpaka Juni 2022 ya ufuatiliaji wa utekelezaji wa miradi ya maendeleo inayogramu zaidi ya Bil.10 .
Aidha Ndimbo amesema kuwa katika zoezi la usaili wa makarani wa sensa katika baadhi ya kata mkoani Mbeya kulikuwa na upendeleo kwenye usaili wa makarani ambapo kuna mtendaji na mkuu wa shule ambao waliwapa upendeleo watahiniwa kwa maana kuwa mmoja anapewa maksi nyingi mwingine pungufu ili kuwawezesha waliopewa maksi nyingi waweze kushinda na kushiriki zoezi hilo.
“Lakini kwa taarifa tulizopokea ni kuwa walifanya hivyo baada ya kupokea shilingi laki mbili (20,0000)kwa kila mmoja na kwamba bado tunaendelea kulifanyia kazi suala hili na wasimamizi hawa tayari wameondolewa kwenye usimamizi huo na tumechukua hatua za awali kuhusiana na tukio hili “amesema Ndimbo.
Aidha Mkuu huyo wa Takukuru ametaja wasimamizi hao kuwa ni Mtendaji wa Kata ya Sinde ,Hawa Kajula pamoja na Mkuu wa shule ya msingi Mlimani , Baita Sanga ambapo wote wawili walituhumiwa kupokea rushwa ya 20,0000 kwa kila mtainiwa ili waweze kupewa upendeleo na wapitwishwe kuwa makarani wa Sensa na kwamba uchunguzi wa awali ulifanyika na kubaini kuwa zoezi la usaili kuna baadhi ya watainiwa katika usaili uliofanywa walitoa maksi za pendeleo kwa watainiwa wanne kwa swali lile lile na majibu yale yale huku wengine maksi za juu kwenye usaili huo na chini baada ysa kubaini hayo walichukua hatua za kuwasimamisha kwenye zoezi la Sensa la usimamizi kwa kushirikiana mwajiri.
“Baada ya kubaini hilo tulichukua hatua za kiutawala kwa kushirikiana na mwajiri pamoja na wasimamizi wa Sensa Mkoa na Wilaya kwa kuchukua hatua kwa kuwaondoa kwenye kushiriki zoezi la Sensa kwa kutokuwa wasimamizi wa Sensa ambao ni Hawa Idd na Baita Sanga waliondolewa na nafasi zao kubadili watu wengine “amesema Mkuu huyo wa Takukuru.
Akifafanua zaidi Ndimbo amesema kuwa kwa watahiniwa ambao walipendelewa kwenye usaili wa zoezi la sensa walinyimwa sifa za kuchaguliwa na wale ambao walipunjwa maksi walipewa sifa za kuchaguliwa kuwa makarani wa Sensa.
“Kwa upande wa Rushwa bado hatujaweza kupata ushahidi wa wazi hili bado tunachunguza kwenye simu zao miamala iliyoingia ili tuone kama kuna fedha ziliingia na kama tutabaini watafikishwa mahakamani ,lakini kama hatutabaini kuwepo kwa tukio la kupokea rushwa tunakusudia kupendekeza hatua za kiutawala zaidi dhidi yao kwani kitendo walichofanya kilikuwa na lengo la kuharibu zoezi la sensa, kwa maana ya kuondolewa tu hakitoshi hizi zilikuwa hatua za awali zilizochukuliwa lakini baada ya kukamilisha uchunguzi wetu tutatoa mapendekezo ya kiutawala”amesema Mkuu wa Takukuru.
Aidha Ndimbo ametoa rai kwa wadau wote wa sensa kujiepusha rushwa na udanganyifu au kutumia nafasi ya usimamizi wa sensa kushiriki vitendo vya rushwa ,wananchi kuwa makini na mtu wa sensa anapokuja lazima awe na kiongozi husika wa eneo ili kukwepa udanganyifu ,lakini pia vifaa vyote vya sensa walivyopewa makarani ni vema wakavitunza kwa umakini mpaka zoezi hilo litakapokamilika kwani ikibainika vimepotea zoezi zima linaharibika.
0 Comments