Na Hamida Ramadhan Matukio Daima APP Dodoma
Mtakwimu Mkuu wa wa Serikali Dk.Albina Chuwa ameyasema hayo leo Jijini hapa Mtakwimu huyo alisema hatua hiyo iliyobaki itakwenda kukamilika hadi tarehe 2 2022 September na zoezi hilo litafanyika kwa njia ya simu zilizotolewa zitatumika kuwafikia ambao hawajahesabiwa .
Dkt Albina Chuwa alisema utaratibu Maalum utaandaliwa wa namna ya kuzifikia Kaya hizo kupitia Viongozi wa mitaa na vitongoji
Kwa Upande wa sensa ya majengo ambayo ilianza jana Dkt Chuwa amesema hadi kufikia Agosti 31 mwaka huu jumla ya majengo yalikwisha hesabiwa ni Milioni 6,351,927 ambapo taarifa ya umiliki ,mahali yalipo na taarifa nyingine zilizoainishwa katika Dodoso la Majengo zimekusanywa.
" Kwa makadrio ya Oparesheni Anwani za makazi tunategemea kuhesabu majengo yapatayo Milioni 12.7 kwa nchi mzima," alisema Dkt Chuwa.
Na kuongeza" Kama tunavyofahamu Serikali kwa Mara ya kwanza tangu tupate Uhuru mwaka 1961 sensa ya Watu na makazi ya kidigitali ambayo imejumuisha sensa ya majengo na sensa ya Anwani za makazi katika Mfumo wake wa utekekezaji.
UTOFAUTI YA SENSA YA WATU MAKAZI NA SENSA YA MAJENGO
Dkt Chuwa alieleza Sensa ya Watu na makazi hapa nchini hufanyika kwa mujibu wa Sheria ya takwimu Sura 351 kifungua kidogo Cha 6(2)(a) sensa ya Watu na makazi ya mwaka 2022 na Kama zilivyikuwa sensa nyingine zilizokwisha kufanyika hutumia miongozo ya Umoja wa mataifa kwa Kuwa matokeo yake yanatumika kitaifa na Kimataifa.
Hata hivyo Dkt Chuwa alibainisha sensa ya majengo Dodoso lake linamaswali 27, taarifa zinazokusanywa zinazohusu aina na sifa za Majengo,idadi ya majengo na Nyumba (unit)zilizopo ,hali ya ujenzi /ukaazi na sababu za jengo kutumika.
Alisema ubora , umiliki na jina la Mmiliki wa jengo matumizi ,upaji na uwepo wa nyaraka za kisheria za Mmiliki halikadhalika taarifa kuhusu vifaaa vya ujenzi ikiwemo kusakafia ,kujengwa kuta na kuezekq Pamoja na huduma nyingine zilizomo katika jengo zinazoendelea kukusanywa nchi nzima.
"Kuhusu Bajeti ya sensa ya Watu na makazi na sensa ya Majengo inayoendelea nchi mzima kwamba Bajeti iliidhinishwa na bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa mwaka wa Fedha 2022/2023 ni kiasi Cha TSHs Bilioni 400 sawa na wastani wa TSHs.6,265 au dola za kimarekani (USD) 2.7 kwa mtu mmoja," alisema Dkt Chuwa
0 Comments