NA HADIJA OMARY, LINDI.
MAHAKAMA ya hakimu mkazi wa Mkoa wa Lindi, imehairisha kesi ya mauwaji ya mfungwa Abdalah Ngulumbale inayowakabili maofisa watatu wa magereza mkoani lindi akiwemo mkuu wa gereza la liwale CP Gibriel Sindani kutokana na upelelezi kutokamilika
Hii ni mara ya tatu kwa watuhumiwa hao kufikishwa mahakamani hapo ambapo kwa mara ya kwanza walifikishwa mahakani Juni 23 mwaka huu na leo wamefikishwa mahakamani na kesi yao kuhairishwa mpaka August 3 mwaka huu huku watuhumiwa wa kesi hiyo wakilazimika kusalia rumande
Kesi hiyo yenye namba RMPI 1 ya mwaka 2022 iko chini ya hakimu mfawidhi wa mahakama ya mkoa wa Lindi Consolatha Singano.
Watuumiwa wengine wa kesi hiyo ni pamoja na Sajent Yusuph Athumani na Coplo Fadhili Afwad
Mwishoo
0 Comments