Na MatukioDaimaApp Dar es salaam
Bodi ya korosho Tanzania (CBT) imehamasisha watanzania kilima zao la korosho kwaajili ya kujinufaisha kiuchumi na kuongeza thamani kwa kuzibangua ili kupugunza uuzwaji wa korosho ghafi nje ya nchi.
Akizungumza katika maonyesho ya kimataifa ya kibishara katika viwanja vya sabasaba Kaimu Meneja wa Bodi ya korosho Tanzania Tawi la Dar es salam Jafari Makata alisema kuwa zipo fursa nyingi watanzania wanapaswa kuzichangamkia kwaajili ya uwekezaji.
“Uwepo wetu katika maonyesho haya ni kwaajili ya kuzitangaza fursa mbalimbali kwenye zao la korosho za uwekezaji ndio maana tumekuja hapa leo kuzitangaza ili watanzania kwanza wazifahamu pili waweze kunufufaika nazo ”
“Lengo letu ni kuhakikisha kuwa zao la korosho linaongeza fedha za kigeni na kukuza uchumi wa taifa kwaanza kubangua na kuuza korosho zilizobanguliwa na kwa wakulima wa zao hilo nchini ambapo kwa sasa zaidi ya mikoa 17 inalima zao hilo hivyo fursa kuongezeka zaidi” alisema Matata
0 Comments