Header Ads Widget

WAZIRI DKT CHANA AAGIZA VIONGOZI WA VIJIJI VINAVYOZUNGUKA SHAMBA LA SAO HILL KUSHIRIKIANA KUPAMBANA NA MAJANGA YA MOTO

Mtendaji mkuu  wa wakala wa Huduma za Misitu Tanzania ((Tanzania Forest Services (TFS)

Prof. Dos Santos Silayo akizungumza na  viongozi mbali mbali wa wilaya ya  Mufindi ,Kilombero  ,Kilolo  na Njombe  jana  wakati wa uzinduzi wa kongamano  la mikakati ya kuthibiti majanga  ya  moto wilaya ya  Mufindi  Leo  ,kongamano lililofanyika ukumbi wa  CCM wilaya ya Mufindi 



WAZIRI  wa maliasili na  utalii Dkt  Pindi Chana  amewataka   watendaji  wa  kata ,vijiji  na  wenyeviti  wa  vijiji   pamoja na madiwani  katika  mikoa ya Iringa , Njombe na Morogoro  inayozunguka  shamba  la miti  la Taifa  la Sao Hill kushirikiana   kupambana na majanga ya  moto  yanayojitokeza katika maeneo yao  ili  kuepusha hasala  kubwa inayojitokeza  kutokana  na miti  kuteketea kwa  moto  .Mwandishi Francis Godwin MatukioDaimaAPP

Waziri Dkt  Pindi  aliyasema  hayo leo  katika kongamano la mikakati ya  kupambana na moto  ndani ya  wilaya ya  Mufindi ,kuwa  suala la  udhibiti  wa uchomaji  moto  ovyo  ni moja kati ya  maagizo  15  yaliyotolewa na  waziri  mkuu Kasim Majaliwa  wakati  alipokuwa  akihutubia Taifa  kupitia  kilele  cha maadhimisho ya  siku ya mazingira duniani Juni 5  mwaka  huu  jijini Dodoma.

Hivyo   alisema utekelezaji wa maagizo hayo  unapaswa  kufanyika kwa haraka  zaidi na  kila  mmoja  kuwajibika katika  utekelezaji wake na  kuwepo kwa  mikakati  kabambe ya   kudhibiti  majanga ya  moto  katika  maeneo  yote  nchini  yakiwemo yale yanayozunguka  mashamba ya  miti ya Taifa  kama  shamba la  Sao Hill na  mengine.

Waziri  Dkt  Pindi katika   hotuba yake   iliyosomwa na mtendaji mkuu wa wakala wa Huduma za Misitu Tanzania   (TFS  )Prof  Dos Santos  Silayo  alisema  kuwa    si  vema   viongozi  wa  serikali ya  vijiji kuacha  watu  wakipoteza maisha  kwa  presha  inayotokana na uchomaji moto  miti   yao  kutokana na uzembe wa  baadhi ya  watu  wachache .

 Hivyo  alisema  kupitia kongamano  hilo la mikakati ya  kudhibitio   uchomaji moto   ovyo  ni uhakika   kasi ya  uchomaji moto  ovyo  ndani ya maeneo yote yanayozunguka   hifadhi  za  misitu na mashamba ya  watu  binafsi ndani ya  mkoa  wa  Iringa , Njombe na Morogoro  itaendelea  kupungua   kama  si kumalizika kabisa .


Alisema  kuwa   serikali   kupitia  wakala wa  huduma  za misitu Tanzania  imewekeza   ardhi  yenye  jumla ya  hekta 135,603 kwa  ajili ya  uhifadhi   na upandaji wa miti katika shamba la  sao Hill   kuwa  serikali  imeweka mikakati ya  kupanda  miti  kwa  awamu  kulingana na mipango  iliyowekwa .


" Wananchi  baada ya  kuona  maeneo ya shamba la Miti  Sao Hill yako  wazi  wameanza   kuvamia  kwa  shughuli  za  kilimo ,upandaji  miti  na maeneo mengine  kuweka  makazi ,kutokana na hilo  serikali  imeanza  kutatua  mgogoro  huo  kwa  kuainisha wavamizi  kwenye  vijiji  12"  ikumbukwe   kuwa  maeneo hayo  yapo  kwenye mipaka  iliyopimwa  ,hivyo  hata ukivamia  zile  alama  hazitoki  jambo la  msingi  ni  wananchi  kuacha  kuvamia maeneo hayo" alisema  waziri Dkt  Chana 

 Kwa  kwa mujibu wa  taarifa za  awali  ya  tathimini  na utambuzi  wa  maeneo yaliyovamiwa  ilithibitisha  kuwa   jumla ya  Hekta  3,617.7 zimevamiwa    wakati  jumla ya wavamizi 962 waliweza  kutambuliwa   kwenye  vijiji  ambavyo vilikubali  kufanyiwa  tathimini  na utambuzi  wa maeneo yaliyovamiwa  katika  Hifadhi  za misitu  zinazopakana na  vijiji  hivyo .

Alisema  kwa  ujumla takwimu  za  aina ya  uvamizi  ilikuwa ni  makazi  asilimia 17  ,kilimo asilimia 16 na upandaji miti ya  biashara  asilimia 67 kwa sasa  vijiji vya  kibengu na usokami havijafanyiwa  tathimini  kwa  sababu ya  wananchi   hawajajitokeza  kufanyiwa  tathimini  hiyo.

 Alisema serikali  itaendelea kulinda  eneo lake kulingana na mipaka iliyopo   kisheria hivyo kuwaomba wenyeviti wa maeneo hayo  yanayozunguka  maeneo ya  shamba la  Sao Hill na maeneo yote ya  hifadhi  kusaidiana kutoa  elimu kwa wananchi  ili pasiwe na uvamizi .


Aidha  alisema  hivi karibuni suala la  wizi  wa miti  limeanza  kujitokeza kwa  watu  kuvuna  miti ya  makampuni ,watu  binafsi   na taasisi  mbali mbali  katika  wilaya ya  Mufindi  kitendo  cha  kuiba miti  mashambani  kinarudisha  nyuma  maendeleo  kwa  waliopanda  na kutunza  miti   hiyo.


Pia  alisema  wizi  huo  unawakatisha  tamaa  wadau  wa miti  lakini  bado  kuna maswali  ya kujiuliza   kwanini  wizi  wa miti  unatokea  sasa na jibu lake  ni  moja  kuwa   thamani ya  miti  imeongezeka hivyo  jitihada  za  uhamasishaji  wananchi  upandaji  miti  katka  ardhi  zao  unajitajika  kuendelea  zaidi  ndani ya mkoa wa Iringa na  Njombe pamoja na mikoa mingine ambayo  hali ya hewa inaruhusu  kilimo cha miti.


Awali  mkuu  wa wilaya ya  Mufindi  Saad Mtambule  akimkaribisha   mgeni rasmi  alisema kuwa  wilaya ya  Mufindi  imeweka mikakati  mbali mbali ya kupambana na majanga ya moto na moja kati ya mikakati yake ni  kufanya kongamano  hilo la  wadau  wa  sekta ya misitu ili  kujiandaa kupambana na majanga ya moto  pindi yanapojitokeza .


Kwa  upande wake  meneja mkuu  wa kampuni ya Green Resources Ltd ( GRL)   Hampus Hamilton alisema kuwa  tathimini  ya kampuni yake imebaini kubwa  miti yenye  thamani ya  shilingi biloini 10  ambayo ni miti ya makampuni ,taasisi na  watu  binafsi  pamoja na shamba la Miti Sao Hill  imeteketea kwa  moto  kwa  kipindi  cha mwaka mmoja  pekee .


Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI