NA HADIJA OMARY ,MATUKIO DAIMA APP LINDI
WAZIRI wa Habari, Teknolojia na mawasiliano Nape Nnauye ameupongeza mkoa wa Lindi kwa kufanya vizuri katika zoezi la uwekaji wa Anwani za makazi na Post Code na kubaki katika nafasi kumi bora kwa mikoa yote nchini Tanzania tangu kuanza kwa zoezi hilo.
Ameyasema hayo akiwa katika ziara ya ukaguzi wa zoezi hilo mkoani Lindi ikiwa ni muendelezo wa zihara yake ya kukagua zoezi la uwekaji anuani za Makazi Nchi Mzima
Waziri Nape alitumia nafasi hiyo kuwashukuru viongozi na wananchi wa Mkoa huo kwa ushirikiano waliouonyesha kwani kufanya vizuri kwa Mkoa huo ni heshima kwake kwa kuwa jimbo lake lipo Mkoa wa Lindi.
"nafasi ya Mkoa kufanya vizuri, katika zoezi hili la anuani za makaazi limeniheshimisha kwanza mimi mwenyewe kama Mbunge wa jimbo la Mtama linalopatikana katika Mkoa huu wa Lindi Pamoja na Waziri Mkuu Kasimu Majaliwa ambaye ni Mwenyekiti wa kamati inayoendesha na kuratibu zoezi la Anwani na Post Code hapa Nchini.
Aidha Waziri Nape amewataka viongozi kufanya maamuzi ya kutoa Majina ya mitaa yatakayoenzi Historia ya Mkoa na viongozi mbalimbali licha ya wananchi kuwa na nafasi ya kupendekeza majina ya mitaa yao.
Awali Mkuu wa wilaya ya Lindi Shahibu Ndemanga akimuwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Lindi Bi. Zainab Telack, akieleza mwenendo wa zoezi la uwekaji wa anuani za Makaazi na post code alisema kuwa zoezi wakati zoezi hilo linaendelea mbali na kutengeneza ajira kwa vijana waliohusika , pia imesaidia kujenga mahusiano na taasisi zingine.
0 Comments