Na, Titus Mwombeki- MTDTV BUKOBA.
Wafanyabishara mkoani Kagera wametakiwa kukaa tayari kwaajiri ya kuanza kutumia mfumo mpya wa uwasilishaji wa mfumo mpya wa kielekroniki wa ritani unaotegewa kuanza kutumika mwanzoni mwa mwezi wa Machi mwaka huu.
Kauli hiyo imetolewa na afisa huduma wa TRA mkoa wa kagera Alex Mwambenja wakati akitoa elimu kwa wafanyabiashara wa halmashauri ya Manispaa ya Bukoba namna ya kutumia mfumo huo utakao saidia kupunguza changamoto mbalimbali ikiwemo wafanyabishara kupigwa faini pindi wanapochelewa kulipa kodi kwa wakati kwa sababu mbalimbali.
“ Tumewaomba wafanyabiasha kuwa na kompyuta ambazo zinatumia mfumo wa ‘exel’ ya kuanzia 2010 hii itawasaidia kuwasilisha ritani kwa usahihi zaidi, tunawakumbusha pia wafanyabiashara waweze kuwasilisha makadilio yao yote ya mapato kabla ya tarehe 31 mwezi Machi ili kuepusha faini ambazo sio za lazima ambazo wanaweza kupiwa na TRA endapo watachelewa kutunza taarifa zao kwa wakati”
Amesisitiza kuwa, wafanyabishara wote hasa wale wanaofanya biashara kutoka nje ya nchi kuakikisha wanapoenda kununua bidhaa wawekewe TIN zao wakati wa manunuzi.
“Mfanyabiashara yoyote ambaye hatawekewa TIN yake pamoja na namba ya kudhibitisha wakati wa manunuzi ya bidhaa yake, lisiti hiyo aitatumika kwenye madai ya kodi ya ongezeko la thamani”
Kwa upande wake Ibrahimu Sokwala ambaye ni mfanyabiashara katika halmashauri ya Manispaa ya Bukoba, ameishukuru taasisi ya ukusanyaji mapato TRA mkoani kagera kwa utoaji wa elimu juu ya mfumo mpya wa kielekroniki wa uwasilishaji wa ritani ya VAT na kuwaomba TRA kuendelea kutoa semina kama hizi kwa wafanyabiashara kwani zinawasaidia kuongeza uelewa.
“Sisi kama walipakodi tunafurahi sana tunapopatiwa semina kama hizi, mfano wafanya biashara wengi kabla ya kupatiwa elimu juu ya mfumo huu mpya unaoenda kutumika tulikuwa tunajiuliza maswali mengi hasa kama tutaweza kuumudu lakini kupitia semina hii ambayo tumepatiwa tumejifunza na kupatiwa majibu ya maswali mbalimbali ambayo yalikuwa yakitutatanisha”
0 Comments