Header Ads Widget

RUFAA YA KIJANA ALIYELAWITI MTOTO YAMPONZA AHUKUMIWA KIFUNGO CHA MAISHA JELA ...



Mahakama ya rufaa ya jamhuri ya muungano wa Tanzania Iringa imetoa maamuzi katika shauri la rufaa No. 31 la mwaka 2020, rufaa hii ilikuwa baina ya Isaya Msofe (mkata rufaa)  dhidi ya Jamuhuri.

Katika maamzi ya mahakama ya rufaa imeamuru mleta rufaa kwamba rufaa yake imeshindwa na ameamuliwa kutumikia kifungo cha maisha jela.

Mwenendo wa kesi hii ulikuwa kama ifuatavyo; awali mkata rufaa  Isaya Msofe alishitakiwa na Jamhuri katika wilaya ya Mufindi tarehe 08/03/2019 kwa kosa la ulawiti (unnatural offence) kinyume na kifungu cha 154(1)(a) cha sheria ya kanuni za adhabu sura ya 16 marejeo ya mwaka 2012 kwa wakati huo na sasa ni marejeo ya mwaka 2019.

Mshitakiwa alipatikana na hatia katika mahakama ya wilaya ya Mufindi na mahakama hiyo iliamuru atumikie kifungo cha maisha jela kwa kosa hilo la kulawiti mtoto mdogo mwenye umri wa miaka 15.

Mshitakiwa hakuridhika na adhabu hiyo hivyo alikata rufaa katika mahakama kuu ya Tanzania Iringa na kusikiliza rufaa yake na mahakama kuu ilitoa uamuzi kwa mkata rufaa kutumikia kifungo cha miaka 30 jela, Bwana Isaya Msofe hakuridhika, hivyo aliamua kukata rufaa katika mahakama ya rufaa ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania kupinga hukumu ya mahakama kuu ya Tanzania, na upande wa jamuhuri haukukubaliana na rufaa yake ulipinga na kudai kuwa mahakama kuu ya Tanzania ilikosa hukumu yake ya miaka 30 jela na kukubaliana na hukumu ya mahakama ya wilaya ya Mufindi kuwa mkata rufaa alistahili kifungo cha maisha jela hivo upande wa jamuhuri ulipendekeza hukumu iliyotolewa mwanzo na mahakama wilaya ya Mufindi isimame, mahakama ya rufaa ilikubaliana na hoja ya upande wa jamhuri hivo imemuhukumu mkata rufaa kifungo cha maisha jela, ili iwe fundisho kwa jamii na watu wote wenye tabia ya kulawiti watoto wadogo.

Pia mkuu wa mashitaka mkoa wa Iringa Bwana Basilius Namkabe amewasihi wazazi wawe makini na watoto wao wafuatilie mienendo ya watoto wao na wawe rafiki wa watoto wao ili hata kama mtoto akipata shida au kufanyiwa kitendo cha ukatili awe tayari kueleza kwa mzazi.

Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI