Header Ads Widget

WANANCHI KIKONGA WAJENGA ZAHANATI, DC MWANGA AWAPA TANO

 


Wananchi wa Kitongoji Cha Kikonga kijiji Cha Kisanga Wilaya Kilosa Mkoa wa Morogoro wameanza ujenzi wa zahanati  ambayo itasaidia kutoa huduma kwa watu zaidi ya elfu tatu


Mwenyekiti wa Kitongoji hicho Christopher Petro amesema ujenzi wa zahanati hiyo umekuja baada ya wananchi kupata changamoto ya kupata  huduma ya afya kwa kutembea zaidi ya kilometa 15 Hadi katika Zahanati ya kijijj na kusababisha baadhi ya akina mama wajawazito kujifungulia njiani 



Petro anasema baada ya kuwepo kwa changamoto hiyo wamekubaliana wananchi kuchangia fedha kiasi Cha  shilingi elfu tano kwa kila mwananchi.


"kila mwananchi amechangia elfu tano ambapo Hadi Sasa tumepata zaidi ya milioni mbili hivyo tuneoba tuanze na msingi huku michango inaendelea" Chistopher Petro mwenyekiti kitongoji Cha Kikonga


Naye Amina Seleman mkazi wa Kijiji hicho anasema licha ya Zahanati hiyo kuwa mbali bado huduma zinazotolewa haziridhishi hivyo kukamilika kwa ujezi wa Zahanati hiyo utaokoa vifo vya watoto na wajawazito



Katika kuunga mkono juhudi za wananchi Viongozi mbalimbali wameahidi kuchangia ambapo  Mkuu wa wilaya ya Kilosa Alhaj Majd Mwanga ameahidi  mifuko ya saruji 64


DC Mwanga anasema lengo la serikali ya awamu ya nne kuhakikisha wananchi wanapata huduma Bora za afya  hivyo watahakikisha Zahanati hiyo inakamilika kwa wakati hivyo ataendela kuchangia Mara kwa mara


Wengine waliotoa ahadi za michango ni pamoja na  chama Cha Mapinduzi wilaya ya Kilosa kimeahidi kutoa  Bati mia mbili na mbunge wa Jimbo la Mikumi Denis Londo akiahidi  mifuko 150 ya Saruji.



Dokta George Kasibante NI Mganga mkuu wa halmashauri ya Wilaya ya Kilosa anasema tayari serikali imeanza mchanakati  wa usajili wa Zahanati hiyo


Dokta Kasibante anasema wananchi wengi wamekua wakijenga vituo vya afya na Zahanati bila kushirikisha uongozi jambo linasababisha ucheleweshaji wa usajili


Zaidi ya asilimia tisini ya ujenzi wa Zahanati hiyo utatumia nguvu kazi za wananchi huku malengo ya serikali kila Kijiji kuwa na Zahanati  ambapo Kijiji hicho kitakua ja Zahanati mbili .



Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI