Header Ads Widget

WALIOSHINDWA KUENDELEZA ARDHI BONDE LA KIRU WAPEWA ONYO


Babati. Waziri Mkuu, Kassimu Majaliwa ameagiza viongozi wa serikali mkoa wa Manyara, kufatilia ardhi ya wawekezaji  ambayo haijaendelezwa katika bonde la Kiru  wilayani Babati,mkoaManyara  ili igawanywe kwa wananchi walio na uhaba wa ardhi ya kilimo na ufugaji.


Katika wilaya hiyo Babati, wananchi wamekuwa na changamoto za  maeneo ya malisho ya mifugo na maeneo ya kilimo na baadhi  kuingia katika maeneo ya hifadhi za taifa na  eneo lhifadhi ya jamii ya wanyamapori ya Burunge.

Akizungumza na wananchi wakati akikagua hospitali mpya ya wilaya ya Babati inayojengwa eneo la Mwada,Waziri Mkuu, alisema wawekezaji wenye ardhi kubwa ambayo hawalimi itarejeshwa kwa wananchi.

Waziri Mkuu alisema changamoto ya ardhi pia ipo katika maeneo ya wilaya za Hanang na Mbulu  hivyo ni lazima ipatiwe ufumbuzi.


Awali Mbunge wa jimbo la Babati,Daniel Sillo alimuomba  WaziriMkuu, kusaidia kugawanywa kwa wananchi,maeneo ya Mashamba ya bondela Kiruambayo hayajaendelezwa.

Katika wilaya Babati, wananchi wamekuwa na changamoto za  maeneo ya malisho ya mifugo na maeneo ya kilimo na baadhi  kuingia katika maeneo ya hifadhi za taifa na  eneo la hifadhi ya jamii ya wanyamapori ya Burunge.

Kutokana na ongezeko la shughuli za kibinaadamu  mapito ya wanyamapori hasa eno la kwakuchinja yamevamia lakini pia maeneo ya Burunge WMA.


Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI