CHAMA cha Mapinduzi (CCM) Kimetaka wanachama na Viongozi mbali mbali ndani ya mkoa huo kuacha kutoa matamko yanayovuruga jitihada za Serikali iliyopo madarakani na kuwa hawatawavulimia wote watakaobainika .
Kuwa chama kina taratibu zake kutumia vikao rasmi na sio kutumia vyombo vya habari kutoa matamko yasiyo na Afya ndani ya chama na Serikali iliyopo madarakani .
Akitoa tamko la CCM mkoa wa Iringa Kwa wanahabari leo Katibu mwenezi CCM mkoa wa Iringa Hilary Kipingi alisema wao kama chama mkoa hawajapendezwa na Kauli iliyotolewa na Spika wa Bunge Job Ndugai ya kupinga jitihada za Serikali kukopa mikopo ya kuendesha miradi .
Alisema Kauli ya Ndugai imelenga kumkwamisha Rais Samia Suluhu Hassan katika kuliletea Taifa maendeleo kuwa wao kama chama mkoa wanapongeza jitihada za Rais Samia Katika kuendelea kutafuta fedha za kuliletea Taifa maendeleo .
Kuwa mikopo ni sehemu ya maendeleo na hata nchi kubwa zimekopa mikopo kama hiyo .
Kipingi alisema kuwa mbali ya kazi kubwa inayofanywa na Rais samia katika ujenzi wa miradi mbali mbali wapo baadhi ya viongozi wanaibuka na kupinga .
Alisema kuwa tangu Rais Samia aingie madarakani mwezi machi mwaka 2021 kumekuwepo na jitihada kubwa zenye mageuzi makubwa katika Taifa na maendeleo makubwa kwa kuwepo kwa mambo makubwa ambayo yamefanyika kwa kipindi cha miezi tisa aliyokuwepo madarakani na kila mmoja ni shahidi kwa kazi hiyo.
“Deni la taifa linakaribia shilingi Tirioni 70 Lakini tutambue kuwa deni la serikali ya awamu ya sita imekuwa ni serikali yenye uwazi zamani ya kwanza hadi ya tano fedha zilikuwa zikikopwa lakini uwazi ulikuwa hauwekwi wazi wala wananchi mlikuwa hamuelezwi serikali imekopa nini na imefanyia nini lakini Mheshimiwa Samia amechukua fedha Trilioni moja na bilioni miatatu fedha ambazo baada ya kuzipata ameshirikisha bunge na viongozi wa serikali pamoja na kufanya kikao kueleza matumizi ya fedha hizo watanzania wote waliona na hili jambo la mfano na la kupongezwa “ alisema Kihongosi
Kuwa iwapo kiongozi mkuu wa nchi anaweza kuchukua fedha na kuainisha matumizi yake kwa mwananchi anajua wazi kuwa fedha iliyokopwa inakwenda kufanya nini .
Alisema faida ya mikopo huo ni kuwa hakuna riba yoyote kwa serikali na ni deni litakalolipwa kwa zaidi ya miaka 20 tena pasipo riba yoyote ile na fedha hizo zimesambazwa kwenye ujenzi wa vyumba vya madarasa na sekta ya afya ,maji na maeneo mengine kila mkoa.
Pia alisema fedha hizo zimeelekezwa kwenye uboreshaji wa miundo mbinu ya barabara kila kona ya nchi hii .
Aidha alisema kwa kipindi kifupi cha serikali ya wamu ya sita madarakani fursa nyingi zimekuwepo kila eneo ambapo kwa vijana wa vyuo vikuu kwenye kipindi cha serikali hii ndipo walipopata mikopo zaidi kuliko wakati mwingine wote kwa mikopo zaidi ya bilioni 570 .
Alisema kuwa kwa miradi inayoendelea nchini ni miradi itakayonufaisha vijana wengi zaidi na wao kama vijana hawatakubali kuona kuna viongozi wanatumia vyombo vya habari kutaka kumkwamisha Rais kwa kumsema vibaya kwa viongozi hao kabla ya hawajafanikisha kumkwamisha Rais watakwamishwa wao maana yeyote anayesimama na kumpinga Rais kwao ataonekana ni adui ni lazima ashughulikiwe .
“ Iwapo wewe ni kiongozi ndani ya nchi hii ama kiongozi ndani ya chama una hoja ya kumshauri Rais ni vema kutumia vikao husika kufikisha ushauri wako kuliko kwenda kwenye vyombo vya habari ama kutumia majukwaa ya nje kumsema vibaya kiongozi huyo hatavumiliwa hata kigodo .alisema Kipingi





0 Comments