Header Ads Widget

BREAKING:MOTO WATEKETEZA JENGO LA BUNGE


Maelezo ya vide


Moto mkubwa unawaka katika jengo la Bunge katika jiji la Cape Town nchini Afrika Kusini.

Picha za video zinaonyesha moshi mweusi mwingi ukijaa angani, huku miali mikubwa ya moto ikitoka kwenye paa la jengo hilo.

Makumi ya wazima moto wako wanaonekana wakipambana na moto huo; bado haijafahamika chanzo cha moto huo.

Tukio hilo linakuja saa chache baada ya mazishi ya Askofu Mkuu Desmond Tutu katika Kanisa Kuu la St George, karibu na bunge.

Smoke rises from a burning building in Cape Town, South Africa, on 2 January 2022, in this picture obtained from social media

CHANZO CHA PICHA,

Maofisa wanasema moto huo ulianzia kwenye ofisi za ghorofa ya tatu na kuenea haraka hadi kwenye Bunge la Kitaifa (baraza kuu la bunge), anaripoti mwandishi wa BBC Nomsa Maseko mjini Cape Town.

Hakuna watu waliojeruhiwa walioripotiwa na hakuna dalili ya kile kilichosababisha moto huo, mwandishi wetu anaongeza.

Maafisa wa kikosi cha zimamoto na uokoaji walisema inaweza kuchukua saa nyingine nne kuzima moto huo kabisa kwa sababu ya mazulia na sakafu ya mbao iko katika jengo hilo.

Waziri wa miundombinu , Patricia de Lille, awali alisema moto katika Baraza la Mikoa (baraza la juu) umezuiwa, lakini bado unaendelea kuwaka Bungeni.

Ruka Twitter ujumbe, 1

Mwisho waMjumbe wa kamati ya usalama Cape Town , JP Smith, aliwaambia waandishi wa habari kuwa paa lilikuwa limeporomoka kwa kiasi na kwamba kengele ya kutambua moto haikulia wakati moto huo ulipoanza kuwaka.

"Paa la jengo limeporomoka upande mmoja na moto umeenea hadi kwa mkutano mpya, kulingana na maafisa.

"Wamegundua nyufa kubwa kwenye ukuta, jambo ambalo linatia wasiwasi.

"Wazima moto wanaripoti kwamba walikuwa kwenye eneo la tukio kwa muda kabla ya mfumo wa kutambua moto kuanza na kisha kutoa tahadhari. Kwa hivyo inaonekana kwamba mfumo huo ulichelewa kwa kiasi fulani."

Hakuna mikutano inayoendelea Bungeni kwa sasa kwa sababu ya likizo.

Firefighters work among the smoke after a fire broke out in the Parliament in Cape Town, South Africa, on 2 January 2022

CHANZO CHA PICHA,

Jengo la Bunge huko Cape Town lina sehemu tatu, na kongwe zaidi ya 1884. Sehemu mpya zaidi zilizojengwa katika miaka ya 1920 na 1980 la Bunge la Kitaifa.

Mwaka jana, moto uliteketeza sehemu ya maktaba ya Chuo Kikuu cha Cape Town, ambayo ilikuwa na mkusanyiko wa kipekee wa kumbukumbu za Kiafrika

Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI