Mkuu wa wilaya ya Iringa Mohamed Moyo wa pili kulia waliokaa akiwa na Viongozi wa taasisi isiyo ya kiserikali ya Brand Tanzania Initiative(BTI) Leo baada ya kufunga mafunzo ya siku tatu jana mjini Iringa kushoto kwake ni Mlezi wa BTI balozi mstaafu wa Madagascar Balozi Rajab Omar Luhwavi
SERIKALI ya mkoa wa Iringa imetaka jitihada zilizoanzishwa na taasisi isiyo ya kiserikali ya Brand Tanzania Initiative(BTI) kwa kutangaza fursa za utalii ndani ya mkoa wa Iringa na Tanzania kuungwa mkono zaidi kwani zinashabiana na mkakati wa Rais Samia Suluhu Hassan wa kutangaza utalii wa Tanzania ulimwenguni kupitia The Royal Tour.
Mkuu wa mkoa wa Iringa Queen Sendiga ametoa Rai hiyo Leo katika ukumbi wa Iringa Sunset wakati akifunga mafunzo ya siku tatau kwa watendakazi wa taasisi ya BTI , alisema kuwa lengo la serikali ya awamu ya sita ni kuona sekta ya utalii inatangazwa zaidi duniani Ulimwenguni kupitia sekta hiyo serikali inakuza uchumi wake kwa watalii zaidi kuja kutalii nchini.
Mkuu wa mkoa ambae aliwakilishwa na mkuu wa wilaya ya Iringa Mohamed Moyo alisema kuwa kuwa moja kati ya maeneo ambayo yanaweza kuvutia watalii wengi zaidi kutembelea vivutio vya utalii ndani ya mkoa wa Iringa ni pamoja na uboreshaji wa miundo mbinu ya viwanja vya ndege kazi ambazo kwa mkoa wa Iringa imeendelea kufanyika kwa uwanja wa ndege Nduli kuboreshwa na ifikapo mwezi macha mwakani uwanja huo utaanza kutumika .
Pia alisema serikali ina mpango wa kuweka kituo cha utalii eneo la Kihesa Kilolo ambacho wakati wowote kituo hicho kitaanza kujengwa kwani mipango yote ipo tayari .
Aidha alisema ipo miradi ya uendelezaji wa utalii mikoa ya kusini (REGROW) inaendelea kazi ikiwa ni pamoja na kusogeza umeme katika hifadhi ya taifa ya Ruaha pamoja na kuboresha barabara ya kuelekea hifadhi ya Ruaha kwa kiwango cha lami.
Alisema jitihada zinazofanywa na BTI zinakwenda sambamba na jitihada za Rais Samia kupitia filamu aliyoirekodi ya The Royal Tour hivyo alisema kama serikali ya mkoa wa Iringa haitakubali kuona kuna mtu anakwamisha jitihada za BTI katika kutekeleza majukumu yake ya kutangaza fursa za utalii ndani ya mkoa huo na fursa nyingine .
Hivyo alisema kupitia maboresho ya uwanja huo ni rahisi kwa watalii zaidi kuendelea kufika kutalii katika vivutio vya utalii ndani ya mkoa wa Iringa na mikoa ya nyanda za juu kusini hasa ukizingatia mkoa wa Iringa ni lango la utalii kwa mikoa ya kusini mwa Tanzania.
Katibu mtendaji wa BTI Lusekelo Mwandemange alisema kuwa taasisi hiyo yenye miaka 9 sasa lengo lake kuu ni kuitangaza nchi kimkakati pamoja na kujenga ushindani wa nchi .
Alisema taasisi hiyo inaundwa na vijana kutoka nchi nzima na kuwa kazi yao kubwa kufanya uchambuzi kitaifa na kimataifa , kuisaidia nchi kusonga mbele kimaendeleo pamoja na kufanya tathimini ya mambo mbali mbali kwa kuhusisha wataalamu mbali mbali .
Akijibu swali la wanahabari kuhusu kauli tata zinazotolewa na baadhi ya viongozi nchini ambazo zinaonesha wazi ninavuruga Taifa , alisema pamoja na kuwa asingependa kujibia nani kasema nini na nani kajibu nini ila kun a shida ya baadhi ya viongozi kupima mambo ya kutoa kwa umma jambo ambalo ni baya sana .
Hivyo wao kama BTI wanaendelea kuwajengea uwezo viongozi na vijana nchini ili kujua nini nchi itataka na kitu gani ambacho si kizuri kwa Taifa .
Katibu huyo alisema tayari BTI wamekwisha andika maandiko kadhaa na kuyapeleka Ikulu wakati wa Serikali ya awamu ya nne chini ya Rais Jakaya Kikwete na kuwa wanampango wa andiko hilo kumpelekea Rais Samia Suluhu Hassan.





0 Comments