Header Ads Widget

"SERIKALI ITAENDELEA KUUNGA MKONO JUHUDI ZA (PSPTB) ZINAZOLENGA KUNGUZA UZEMBE"_RC MONGELA




 


Mkuu wa mkoa wa Arusha John Mongela amesema serikali itaendelea kuunga mkono juhudi  za bodi  ya ununu na ugavi zinazolenga kupunguza au kuondoa kabisa uzembe na ukiukwaji wa maadili katika fani ya ununuzi na ugavi kwani pesa nyingi za serikali zinatumika kupitia taaluma hiyo.



 Mongela aliyasema hayo wakati akifungua  kongamano la 12 la la wataalamu wa ununuzi na ugavi kwa niaba ya waziri wa fedha DkT Mwigulu Nchemba ambapo alisema kuwa bado kuna wataalamu wachache wanafanya  kazi chini ya kiwango cha taaluma yao na kuagiza  bodi ya PSPTB kuendelea  kusimamia taalumu hiyo kwa kuchukua hatua mathubuti kuinua weledi wa wataalamu pamoja na wengine wote wanaoshiriki katika mchakato wa ununuzi na ugavi kwa kuwajengea uwezo katika taratibu za manunuzi na usimamizi wa mikataba .




  Alisema kuwa mada walioiweka katika  kongamano hilo  ambayo inasema kuwa “ubunifu wenye suluhisho katika utekelezaji wa mnyororo  wa ununuzi na ugavi kwa kutambua  ushindani na mapinduzi ya viwanda kwa maendeleo ya jamii  ambapo alibainisha kuwa mada hiyo itaipa changamoto  bodi ya   PSPTB na wataalam kuweza kutambua  umuhimu wao katika utekelezaji wa miradi mikubwa  ya kimkakati inayotekelezwa na serikali ili kuweza kuongeza tija na faida  katika sekta binafsi .



Aidha alisema kuwa waendelee kuchukuwa hatua madhubuti  kwa mtaalamu yeyote anaekiuka kanuni za maadili au kutoa ushauri wa ununuzi kinyume na sheria ya ununuzi wa uma bila uwoga wowote kwani  uzembe na ukosefu wa weledi  katika kusimamia mnyororo wa   ununuzi na ugavi unapelekea kukwamisha utekelezaji wa miradi pamoja na  miradi mingi   kufanyika chini ya kiwango.




Alisema kuwa kuwepo kwa ukiukwaji mkubwa wa maadili kwenye kada hii iwe chachu   ya bodi kuongeza usimamizi wa maadili na kuchukuwa hatua stahiki kwa wahusika kwani taaluma hii ni muhimu sana ili kufikia adhima ya serikali  ya awamu  ya sita ya kuendelea kuwaletea watanzania maendeleo kwa kasi .



Alitoa wito kwa waajiri wote kutoa ushirikiano  kwa bodi haswa linapokuja swala la usimamizi wa taaluma ya ununuzi na ugavi pamoja kuzingatia matakwa yote na sheria za bodi ili kuleta tija ya miradi mbalimbali inayotekelezwa na serikali.


Alisema kuwa katika taasisi nunuzi 85 zilizofanyiwa ukaguzi kwenye viashiria vya rushwa  miradi mitatu yenye kiasi cha shilingi milioni mia  sita kumi na sita nukta tano ilibainika kuwa na viashiria vikubwa vya rushwa ukilinganisha na taarifa ya mwaka 2018\2019 iliobainika  kuwa ukaguzi wa miradi 131 ulionyesha kuwa na miradi 39 ilikuwa na viashiria vya rushwa .


Kwa mujibu wa ukaguzi  uliofanywa na mamlaka ya uthibiti wa manunuzi ya uma  (PPRA) kwa mwaka wa fedha 2020/2021 umethibitisha kuwa ukaguzi wa mikataba 282 yenye dhamani ya shilingi za kitanzania bilioni elfu tano nukta saba na mikataba 281 sawa na asilimia 99.6 imesimamiwa vizuri na kuleta dhamani ya fedha  huku mkataba mmoja ulionyesha kuwa na usimamizi wa  kiwango cha chini  sana .




  Kwa upande wake mwenyekiti wa bodi wa ununuzi na  ugavi (PSPTB)Jacob  Kibona alisema kuwa atahakikisha anasimamia vyema taaluma  na maadili  ya taaluma ya ununuzi  na ugavi ili  kuwezesha taifa kupata dhamani ya kiasi cha pesa kinachoendana na manunuzi  yaliotumika.



Alisema kuwa atafanya kazi kwa weledi uliotukuka kwa kipindi chote  cha nafasi yake  na kumaliza matatizo yote ambapo bodi itahakikisha inachukuwa hatua kali za kinidhamu kwa wataalumu wote watakao sababisha watu kupoteza imani na taasisi hiyo ya ununuzi na ugavi.

 



Naye mkurugenzi mtendaji wa bodi ya PSPTB  Godfred Mbayi alisema kuwa kwa mwaka 2021 imesajili jumla ya wataalam 1166 ambapo wamefanya mitiani  katika hatua tatu bila kutangaza kutokana na kutokuwa na bodi ya wakurugenzi  na idadi hiyo imefanya  idadi ya  wataalamu kuongezeka na kufikia  zaidi ya wataalam  elfu 12000.

Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI