Header Ads Widget

KITUO CHA DBL CHAWAPA FARAJA YATIMA ,ASKOFU MPELI ATOA RAI



WATOTO yatima wa kituo cha Daily Bread Life Ministres cha Mkimbizi katika Manispa ya Iringa  wapewa faraja  ya sikukuu ya Chrismas  kwa  kuandaliwa  chakula cha pamoja na uongozi  wa  kituo  hicho .


Akizungumza mara  baada ya chakula   hicho mkuu  wa  kituo  hicho cha Daily Bread Life Tanzania Askofu Mchungaji Mpeli Mwaisumbe amesema  imekuwa ni kawaida ya  kituo  hicho  kukaa pamoja na watoto hao kula nao chakula na kuwa kila mwaka  wamekuwa  wakifanya  hivyo .

Alisema kuwa pamoja na  kituo  kutekeleza  jukumu lake la  kusaidia malezi ya  watoto  hao  wadau  mbali mbali  wamekuwa  wakiunga mkono  jitihada  za  kusaidia watoto hao akiwemo Geofrey Mungai ambae ni mkandarasi mkubwa Iringa na mkurugenzi wa Hoteli ya Mount Rayol Villa ya  mjini Iringa  ,wanasiasa na na viongozi wa  serikali na wengine .
Askofu  Mwaisumbe  alisema kuwa kituo chake cha DBL kilichopo chini ya  usimamizi wa mchungaji Neema Mwaisumbe kina zaidi ya watoto yatima 40 na kuwa maendeleo ya kituo hicho yametokana na jitihada za wadau mbali mbali ambao wameendelea kujitolea kusaidia kituo hicho.



Wakati  huo  huo Askofu  Mpeli alitoa  rai kwa watendaji wa  kituo  hicho kuendelea kufanya kazi kwa kushikamana  kwa kuheshimu wito walioitiwa na Mungu na kuendelea kuwalea watoto kwa Upendo kwa Mwaka ujao wa 2022.

Aidha alisema kuwa wadau wanaoendelea kusaidia kituo hicho ni wengi zaidi na kuwa kwa umoja wao kituo hicho kinaendelea kuthamini michango yao na kuomba kuzidi kujitolea zaidi kwa ajili ya watoto hao kwa ajili ya kuona watoto hao wanapata elimu Kituo hicho ambacho kina zaidi ya miaka 15 15 toka kuanzishwa kwake kimefanikiwa kuanzisha shule yake ya Sekondari iliyopo kijiji cha Mgera ambayo inapokea na watoto wengine kwa kuchangia ada ndogo zaidi kuzindua shule ya sekondari .






kama umeguswa na jitihada za wale wote wanaojitolea kusaidia yatima wa kituo hiki cha DBL mkimbizi Iringa unaombwa kuchangia mchango wako wowote kupitia namba hii ya mkurugenzi mtendaji wa kituo hiki mchungaji Mpeli kupitia huduma ya TIGO PESA 0719239936 na M-PESA ni 0754362536 na Mungu atakubariki na kukuongezea pale ulipopunguza.





Wageni  mbali mbali  walioshirikia  chakula na yatima  wa  DBL 

Mchungaji Neema Mpeli  akitoa neno 
















Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI