Header Ads Widget

MALALAMIKO 72 YAPOKELEWA TAKUKURU MTWARA

Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (PCCB) Mkoa wa Mtwara imepokea malalamiko 72 huku malalamiko 35 yakihusishwa na rushwa huku malalamika 37 hayakuhusu rushwa. mwandishi wa matukio daima Florence Sanawa anasimulia kutokea Mtwara

Akizungumza na waandishi wa habari Kamanda wa Takukuru Mkoa wa Mtwara Enock Ngailo alisema kuwa katika malalmiko hayo 35 yalifanywa uchunguzi ili kudhibitisha  makosa ya rushwa na uchunguzi wake bado unaendelea.

Alisema kuwa katika malalamiko 37 ambayo hayakuhusu rushwa matano yalishauriwa kuhamishiwa katika idara zingine kwa ufuatiliaji zaidi.

Ngailo alisema kuwa taasisi  zinazolalamikiwa ni halmashauri zinaongoza kwa makosa 33, Vyama vya ushirika  14, maji 3 polisi 3 benki 2 mahakama 1 bima 1 tanesco 1 tanroad 1 na sekta binafsi 1.

Katika kipindi cha kuanzia Julai mwaka huu hadi Septemba walifatilia matumizi ya fedha za umma  katika utelekezaji wa miradi ya maendeleo, ambapo baada ya uchunguzi huo ilibanika kuwepo kwa mianya ya rushwa ambayo imefanyiwa kazi katika vikao vya wadau na kutoa elimu kwa lengo la kuimarisha usimamizi wa  miradi hiyo.

“tulifanikiwa kufatilia miradi ya maendelo mitano ambayo ipo mtwara DC ujenzi wa vyumba viwili vya madarasa na ofisi ya mkuu wa shule msijute kwa gharama zaidi ya shilingi milioni 44, mtwara manispaa ukarabati wa barabara ya jamuhuri chuno, Ghana na Aghakhan ambayo imegharimu  zaidi ya shilingi milioni 351,  tandahimba  ujenzi wa nyumba nne za walimu shule ya msingi kuchele uliogharimu zaidi ya shilingi milioni 100, wilaya ya masasi mradi wa maji kanyimbi masuguru zaidi ya shilingi milioni 405  pamoja na mradi wa ujenzi wa wodi tatu katika hospitali ya wilaya ya masasi milioni 500.



Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI