Header Ads Widget

TWIGA AFA KWA KUPIGWA NA SHOTI YA UMEME

 


SIHA

Mapema leo Oct 10 majira ya saa 1:00 asubuhi katika mashamba ya Nafco kijiji cha Ngarenairobi wilaya ya Siha mnyama aina ya twiga amekufa baada ya kupigwa na umeme akitokea kwenye ushoroba wa hifadhi ya mlima Kilimanjaro


Kamanda wa polisi mkoa wa Kilimanjaro ACP Simon  Maigwa amesema kutokana uhaba  wa maji wanyama wamekuwa wakihama kutoka eneo moja kwenda lingine kutafuta maji na ndivyo kama huyu twiga alivyokatiza kwenye nyaya za umeme na kusababisha kifo chake na kuwa kipindi hiki cha kiangazi wananchi wachukue tahadhari



Wakati huo huo mtuhumiwa mmoja anayehisiwa  kuwa na ugonjwa wa akili katika eneo la Samana kijiji cha Mese wilaya ya Siha amemuua kwa kumkata na kitu chenye ncha kali mtoto Johson Ronald Munuo(6)na kisha kuua ndama kwa kutenganisha kichwa


Kamanda Maigwa amesema mbinu aliyotumia nikuchukua panga linalotumika kukatia majani ya ng'ombe na akiwa kwenye banda la ng'ombe alimkata ndama shingoni nakufa kisha kuelekea alipokuwa mke wa mtuhumiwa akinywa chai  na kutekeleza mauaji ya mtoto huyo


.

Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI