Header Ads Widget

MFUMUKO WA BEI WA TAIFA WAONGEZEKA HADI 4%

 


Na Hamida Ramadhan ,Dodoma 


MFUMUKO wa bei wa Taifa kwa mwaka ulioishia Septemba 2021 umeongezeka hadi asilimia 4.0 kutoka 3.8 kwa mwaka ulioishia mwezi Agosti 2021.


Akiongea na waandishi wa Habari leo Mkurugenzi wa Sensa za watu na Takwimu za Jamii  Ofisi ya Taifa ya Takwimu Ruth Minja amesema hilo ni badiliko la asilimia 0.2 ikilinganishwa na nchi jirani kama Kenya na Uganda ambapo septemba 2021 umeongezeka kwa asilimia 0.3 kwa kila moja kukiwa na maana kuwa kuongezeka huko kunaashiria kasi ya bei za bidhaa na huduma kwa mwaka ulioishia septemba 2021 imeongezeka ikilinganishwa na kasi iliyokuwepo agosti mwaka huu.


Amesema kuongezeka kwa mfumuko wa bei kwa mwaka ulioishia Septemba 2021 kumechangiwa na kuongezeka  kwa mfumuko wa bei wa baadhi ya bidhaa za vyakula  na bidhaa zisizo za vyakula kwa Mwezi  Septemba, 2021 ikilinganishwa na mwezi Septemba  2020


"Kwa baadhi ya bidhaa za vyakula zilizo changia kuongezeka kwa mfumuko wa bei ni pamoja na unga wa ngano 6.8, nyama ya ng’ombe3.4, maziwa

ya unga 9.2, mayai 5.0 na viazi mviringo 4.7 ," amesema Minja


Kwa upande mwengine amesema  baadhi ya bidhaa za vyakula zilizochangia kuongezeka kwa mfu.uko wa bei  nipamoja na gesi ya kupikia kwa asilimi 2.7 mkaa kwa asilimia 3.5 na

huduma ya malazi kwenye nyumba za kulala wageni kwa asilimia 5.7.


Hata hivyo amesema mfumuko wa bei wa taifa kwa mwezi septemba 2021 wa

asilimia 4.0 bado upo ndani ya lengo la serikali la muda mfupi na wa

kati wa kuwa na mfumuko wa asilimia 5 ambao unawezesha shughuli za

kiuchumi kufanyika bila athari, na kwamba serikali inaendelea kufanyia

kazi changamoto zinazofanyia bei na huduma kupanda.


Kwa upande wa nchini Kenya mfumuko wa bei umeongezeka hadi asilimia 6.91kwa mwaka ulioishia mwezi Septemba 2021 kutoka asilimia 6.57 kwa mwezi agosti 2021 huku nchi ya 

Uganda ukiongezeka hadi asilimia 2.2 kutoka asilimia 1.9.

Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI