Header Ads Widget

HAKUNA VITA NZURI, TUILINDE AMANI YA NCHI YETU- MOSHI


Mfanyabiashara ndogondogo wa Mitaa ya Kongo na Pemba, Kariakoo Jijini Dar Es salaam Bw. Elia Moshi amesisitiza kuwa mara zote haki huwa haidaiwi kwenye machafuko na ghasia, akitoa wito wa Vijana kufikiri juu ya athari za machafuko kabla ya kujiingiza kwenye Hamasa zinazotolewa kwenye Mitandao ya Kijamii na baadhi ya watu wasioitakia mema Tanzania.

Bw. Moshi ametoa kauli hiyo wakati akizungumza na waandishi wa habari Mkoani Dar Es Salaam, siku tatu mara baada ya hali ya ulinzi na utulivu kurejea katika maeneo mengi nchini mara baada ya ghasia na fujo zilizojiri kwenye Miji mbalimbali nchini wakati wa uchaguzi Mkuu wa Tanzania Jumatano ya Oktoba 29, 2025.

"Vijana niwaaambie kuwa hakuna Vita nzuri, Vita vina athari kubwa hasa kwetu sisi wa kipato cha chini. Wanaohamasisha Vijana kuingia barabarani wana maisha yao mazuri na hutowaona barabarani ni muhimu kutathmini wale wanaohamasisha ghasia hizo na athari zake kabla ya kuchukua maamuzi." Amesema.

Akizungumzia athari za ghasia hizo, Moshi amesema uchumi ulidorora na kusababisha mfumuko wa bidhaa muhimu za kila siku, akisema kukosa utamaduni wa kuweka akiba kwa Watanzania wengi kumekuwa sababu pia ya wengi kuathirika kutokana na kukosa akiba ya chakula kwenye nyumba zao.



 

Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI