Na Shemsa Mussa -Matukio Daima
Kagera.
Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum, Amos Mpanju, amekabidhi pikipiki tisa (9) kwa halmashauri za Bukoba, Missenyi, na Ngara mkoani Kagera, zitakazotumika kuwawezesha maafisa maendeleo ya jamii kufika kwa urahisi zaidi katika maeneo ya vijijini.
Akizungumza wakati wa makabidhiano hayo, Mpanju alisema hatua hiyo ni sehemu ya jitihada za serikali kuhakikisha huduma za maendeleo zinawafikia wananchi hadi ngazi ya kitongoji, kijiji, mtaa na kata.
> “Division za maendeleo ya jamii zina jukumu la kufanya kazi pamoja katika kusikiliza, kuelimisha, na kusaidia wananchi kuwa na maendeleo yao wenyewe,” alisema Mpanju.
Amesisitiza kuwa maendeleo ya kweli yanapatikana pale wananchi wanaposhiriki kikamilifu katika miradi ya serikali na kujiona kuwa sehemu ya wamiliki wa huduma zinazotolewa.





0 Comments