Header Ads Widget

ONE ONE ANIMAL,SOWETO,AZANIA BANKI YAWAFIKIA WANANCHI NANENANE KANDA YA MASHARIKI

Na Lilian Kasenene,Morogoro

Matukio DaimaApp 

WAFUGAJI wa kuku wametakiwa kutumia chakula sahihi kwa ajili ya mifugo yao ili mfugaji aweze kuinuka kiuchumi na kuendesha maisha yao ya kila siku mfugaji.

Daktari wa kampuni ya uzalishaji wa chakula cha kuku One One Animal Feeds Dk Dioniz Leonard ameeleza hayo wakati akizungumza na waandishi wa habari kwenye maonyesho ya kilimo,ufugaji na uvuvi kanda ya Mashariki.

Dk Dioniz alisema chakula hicho kinamsaidia mfugaji mdogo kuhakikisha anakuwa mfugaji bora na wa kisasa kwani kwa kuanzia na kuku 100 ana uwezo kufikia malengo na tija ina hiyo inamsaidia kuepukana na changamoto za magonjwa.

“Sisi One One tupo kwa ajili ya kumuinua mfugaji wetu na  wafugaji kunawatembelea na kumpa elimu ili aweze kumudu ghrama,kuepuka magonjwa ya kuku na yanayosababishwa kufa na kumpa hasara mfugaji,”alisema

Katika maonyesho hayo Meneja wa Azania Benki Morogoro Makalla Mbura akizungumza mara baada ya banda la benki hiyo kutembelewa na mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam Albert Chalamila alisema benki hiyo ni ya kizalando imekuwa mstari wa mbele kwenye sekta ya kilimo kwa kukopesha wakulima kwenye shughuli za shamba ikiwemo wakulima wa mbogamboga na matunda.

Alisema mkopo wanaotoa hauna ukomo na kwamba kikubwa ni katika kuhakikisha mkulima anafaidika na kuongeza thamani ya kile anacholima.

“Tumekuwa tukikopesha wakulima kwa ajili ya shughuli za shamba lakini pia katika ununuzi wa vifaa na zana za kilimo kama trekta na kwenye mifugo,”alisema meneja huyo.

Kwa upande wake afisa masoko kutoka Soweto Village Hotel Bertha Simon ali[poyte,mbelewa na mkuu huyo wa mkoa wa Dar es Salaamu alieleza kuwa wamekuwa wakitoa huduma mbalimbali za waoto,vijana na watu wazima ikiwa ni pamoja ku kumuweka mtu kwenye hali ya afya anapofanya kazi na kuchoka.

Bertha alisema uwepo wa hoteli hiyo ya Soweto kwenye eneo la Madaganya kata ya Mindu kumeweza kuongeza uchumi kwa mwananchi mmoja mmoja kutokana na wageni  wanaofika hapo kwa ajili kupata huduma.

Mkuu wa mkoa wa Dar es Salaamu Albert Chalamila akitembelea mabanda mbalimbali kwenye maonyesho hayo aliwataka wananchi wa kanda hiyo ya mashariki kutembelea maeneo mbalimbali kwenye maonyesho hayo ili kujifunza zaidi masula ya Ufugaji, ukulima,uvuvi  ama usindikaji wa mazao mbalimbali.


 

Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI