Marekani itawataka raia kutoka Malawi na Zambia kulipa amana ya $15,000 (£11,300) kwa viza ya utalii au biashara, kulingana na Wizara ya mambo ya nje ya Marekani.
Mpango wa majaribio wa miezi 12 unalenga kuzuia mtindo wa kukawia "au pale ambapo habari za uchunguzi na uhakiki zinachukuliwa kuwa duni ", kulingana na ilani iliyochapishwa na wizara ya mambo ya nje.
Maafisa wanasema kwamba raia wa mataifa mengine kando na Malawi na Zambia wanaweza hivi karibuni pia kuhitaji kulipa amana kama hiyo, ambayo itarejeshwa mwishoni mwa ziara yao nchini Marekani.
Utawala wa Marekani umechukua hatua kadhaa kuendeleza ajenda ya Rais Donald Trump ya kukomesha uhamiaji haramu.
Trump alitia saini agizo kuu katika siku ya kwanza ya muhula wake wa pili kwa ajili ya kutekeleza hili.
Taarifa ya wizara ya mambo ya nje, iliyochapishwa Jumanne, inasema: "Wageni wanaoomba viza kama wageni wa muda, kwa biashara au starehe (B-1/B-2) na ambao ni raia wa nchi zilizotambuliwa na Wizara kuwa na viwango vya juu vya gharama za viza, ambapo habari ya uchunguzi na ukaguzi inachukuliwa kuwa duni, ikiwa mgeni alipata uraia bila mahitaji ya ukaaji, inaweza kuwa chini ya mpango wa majaribio.
"Maafisa wa ubalozi wanaweza kuhitaji waombaji viza wasio wahamiaji walioko nchini humo kwa dhamana ya hadi $15,000 kama sharti la kupewa viza, kama inavyoamuliwa na maafisa wa ubalozi."
0 Comments