Header Ads Widget

KATIBU MKUU KIONGOZI ZANZIBAR ZENA SAID AWAFUNDA WANAWAKE VIONGOZI AWATAKA WASIBWETEKE NA VYEO VYAO

Katibu Baraza la Mapinduzi na Katibu Mkuu Kiongozi Zanzibar  Zena Ahmed Said ametoa wito kwa  wanawake  Viongozi  washiriki 70 wa Mafunzo ya Uongozi kutoka katika Taasisi mbalimbali  ambao wanashiriki mafunzo ya uongozi  ya wiki moja   kuwa wasibweteke  na majina ama vyeo vyao huku amewataka wawe na wito wa kujiendeleza wakati wote na kwenda kubadilishana uzoefu na watendaji wenzao.

Katibu Mkuu Kiongozi Zanzibar  amesema  wakati wa  ufunguzi wa mafunzo hayo yanayofanyika kwa mara ya tatu sasa Katika Shule ya Uongozi ya Mwalimu Nyerere Kibaha na Kuongeza Kuwa Watoto wakike wajiamini Katika nafasi mbalimbali wanazopata hasa kwa kuanzia kwenye familia Zao.

Kwa upande wake Mkuu wa Shule ya Uongozi Profesa Marcelina Chijoriga amesema kuwa katika mafunzo hayo yanayoshirikisha  washiriki  kutoka katika Taasisi 19 za serikali huku washiriki wengine wanne  wakiwa wamejilipia wenyewe kutokana na utashi wa kujiendeleza wenyewe.
MERCERINA CHIJORIGA  Mkuu wa Shule ya Uongozi ya Mwalimu Nyerere Kwa Mfipa Kibaha amesema 
baadhi ya washiriki wa Mafunzo Hayo wamesema wanaimani yatawajengea uwezo katika  kazi Zao Pamoja na wale wanaofanyanao kazi kwani wataweza kushirikiana na kubadilishana uzoefu wa kiuongozi.

Mhandisi ANIFA CHINGUMBE-Kaimu Meneja TTCL Kagera ameshukuru kwa Mafunzo ya Uongozi aliyowahi kupata katika Shule ya Uongozi ya Mwalimu Nyerere amepanda cheo.


JULIETH LYIMO Kiongozi wa Mtandao wa Wanawake Mkoa amesema
Mbali ya  kuwa  Shule Uongozi ya Mwalimu Nyerere inatoa mafunzo kwa Vyama na makada wa siasa pia Shule hiyo inatoa mafunzo kwa Taasisi binafsi na hata mtu mmojammoja ambao wanakua wanakidhi vigezo vya kupata huduma .

Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI