Na Matukio Daima App.
Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar imesema kuwa ipo katika hatua za mwisho za kufanya upembuzi yakinifu ya ujenzi wa Daraja linalounganisha Mkokotoni hadi kisiwa cha Tumbatu yenye urefu wa wastani wa kilomita 2.
Aidha Serikali ipo katika za kuanza ujenzi wa Barabara itakayounganisha Mkoa wa Kaskazini Unguja na Mkoa wa kusini Unguja kutoka Nungwi hadi Paje.
Akizungumza na Waandishi wa Habari leo Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Usimamizi na utumzaji aa Barabara Zanzibar Injinia Cosmas amesema Serikali imedhamiria kuunganisha maeneo mbalimbali kwa ujenzi wa barabara na madaraja katika visiwa vidogo vidogo ili kurahisha huduma za usafirishaji nchini.
"Tunasubiri ripoti ya upembuzi yakinifu ili kuona kuna uwezekano wa ujenzi wa Daraja kutoka Mkokotoni hadi Tumbatu ambapo tunaamini ujenzi wa Daraja hili utakifungua zaidi kisiwa cha Timbatu kiuchumi," amesema.
"Kwa sasa tayari tumeshaanza ujenzi wa Barabara zaidi ya kilomita 15 ndani ya kisiwa cha Tumbatu jambo ambalo hakuna alietarajia,"
Ameeleza kuwa, Ilani ya Chama cha Mapinduzi 2025-2030 inawaelekeza kujenga Barabara itakayowaunganisha Wananchi kutoka Kaskazini Unguja hadi Kusini ili kuondia adha ya usafiri pamoja na ujenzi wa barabara za mjini na za ndani katika maeneo ya Unguja na Pemba .
"Muda wowote kuanzia sasa tunaanza ujenzi w Barabara Barabara kutoka Nungwi Kaskazini Unguja hadi Paje Kusini Unguja," ameeleza.
"Kisiwani Pemba hatukuwa nyuma katika utekelezaji wa Ilani maana tuneshakamilisha ujenzi wa Barabara kuu na Barabara za ndani na kutekeleza kwa vitendo Ilani ya chama cha Mapinduzi CCM ya kikufungua kisiwa cha Pemba," Amesema.
Amesema ujenzi wa Barabara ya Wete chake unaendelea kwa kasi huku Ujenzi wa Barabara ya Mkoani Chake - chake ukitarajiwa kuanza hivi karibuni kama Ilani ya Uchaguzi inavyoelekeza.
0 Comments