Header Ads Widget

KATIBU MKUU WA UN ATOA WITO KWA IRAN NA ISRAEL KUKOMESHA MASHAMBULIZI

 

Huku mashambulizi yakiendelea katika eneo hilo, kundi kubwa la viongozi wa dunia linatoa wito wa kupunguza na kujizuia.

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres ametoa wito kwa Iran na Israel kukomesha "ogezeko" la mashambulizi.

''Mashambulizi ya Israeli katika maeneo ya nyuklia ya Iran.Kombora la Iran lililoshambulia Tel Aviv. Ni wakati wa kuacha. Amani na diplomasia lazima ziwepo," anasema kwenye chapisho kwenye X.

Rais wa Tume ya Umoja wa Ulaya Ursula von der Leyen anasema alizungumza na Rais wa Israel Isaac Herzog kuhusu hali inayoendelea. "Nilisisitiza haki ya Israel ya kujilinda na kuwalinda watu wake. Wakati huo huo, kuhifadhi utulivu wa kikanda ni muhimu," anasema kwenye X, akiongeza kuwa amezitaka pande zote "kuchukua hatua kwa kujizuia zaidi".

Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI