Header Ads Widget

JESHI LA ISRAEL LIMESEMA LINAENDELEA NA MASHAMBULIZI DHIDI YA IRAN.

 

Jeshi la Ulinzi la Israel (IDF) linasema kuwa linaendelea na mashambulizi ya anga katika maeneo ya Iran.

Katika taarifa fupi iliyotumwa kwa Telegram, IDF ilisema kwamba "Jeshi la anga la Israel linaendelea kulenga shabaha ili kuondoa vitisho nchini Iran".

Taarifa hiyo ilichapishwa pamoja na video inayoonesha picha za maonyo ya angani.

Hatua hii inakuja zaidi ya saa 24 baada ya shambulio la awali la Israel kwenye kambi za kijeshi za Iran, ambalo liliua makamanda watatu wa kijeshi wa Iran, kulingana na IDF.

Tangu wakati huo Iran imeanzisha mashambulizi ya makombora dhidi ya Israel hadi Jumamosi asubuhi.

Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI