Katika mkutano wa leo wa Kremlin, nilimuuliza msemaji wa Vladimir Putin, Dmitry Peskov, jinsi alivyokuwa na wasiwasi na ukosoaji wa Donald Trump kwa rais wa Urusi, pamoja na maoni yake kwamba Putin alikuwa "mwendawazimu" na mashambulio yake yanayoendelea dhidi ya Ukraine.
Peskov alijibu: "Bila shaka, kuanza kwa mchakato wa mazungumzo, ambayo upande wa Marekani ulifanya juhudi kubwa, ni mafanikio muhimu sana na tunawashukuru sana Wamarekani na binafsi kwa Rais Trump kwa msaada wao katika kuandaa na kuanzisha mchakato huu wa mazungumzo.
"Ni mafanikio muhimu sana. Bila shaka, wakati huo huo huu ni wakati muhimu sana ambao umeunganishwa na mchanganyiko wa hisia wa kila mtu anayehusika.
"Tunafuatilia kwa makini athari zote. Hata hivyo, Rais Putin anachukua maamuzi hayo ambayo ni muhimu kwa usalama wa nchi yetu."Sote tulishuhudia jinsi utawala wa Kyiv ulivyotishia viongozi wa kigeni kabla hawajafika Moscow kuadhimisha Siku ya Ushindi. Kila mtu alisikia vitisho hivi vya utawala wa Kyiv. ''
"Na viongozi wengi waliokuwa hapa walishuhudia majaribio ya utawala wa Kyiv kushambulia eneo la Urusi kwa ndege zisizo na rubani, miji mikubwa, hata mji mkuu, usiku wa kuamkia siku hiyo muhimu.Majaribio haya yanaendelea. Tunalazimika kuchukua hatua na Rais Putin anafanya kile kinachohitajika ili kuhakikisha usalama wa Urusi."
0 Comments