Header Ads Widget

MAKAA YA MAWE, VITO NA DHAHABU KICHOCHEO CHA UCHUMI MKOANI RUVUMA


Makusanyo maduhuli yafikia asilimia 98 kwa mwaka 2024/2025

Ruvuma

MAKUSANYO  ya maduhuli ya Serikali kupitia Sekta ya Madini katika Mkoa wa Ruvuma  yatokanayo na mrabaha, tozo na ada mbalimbali kwa mwaka wa fedha  ulioanza Julai 2024/2025 ni Shilingi Bilioni 32.5.

Fedha hizo ni makusanyo ya mpaka tarehe 19 Mei, 2025 wakitarajiwa kuvuka lengo la fedha walilopangiwa la Shilingi Bilioni 33.15

Akizungumza na  wanahabari wa Tume ya Madini, Afisa Madini Mkazi wa Mkoa wa Ruvuma, Mhandisi Alphonce Bikulamchi amesema, hadi mwishoni mwa mwezi Juni mwaka huu Mkoa huo utakuwa umevuka lengo la zaidi ya  asilimia  100 ya ukusanyaji mapato.


Mhandisi Bikulamchi amesema kuwa mafanikio hayo yamepatikana kutokana na kushamiri kwa biashara ya makaa ya mawe ambayo kwa Mkoa wa Ruvuma yamebainika kuwa ni bora zaidi na yamekuwa yakiuzwa nchi mbalimbali ikiwemo Kenya, Uganda, Rwanda, Bara la Asia na Bara la Ulaya.

Aidha, amesema pia Mkoa huo mbali na makaa  ya mawe pia umebarikiwa kuwa na aina nyingi za madini ikiwemo Dhahabu, Shaba,  Chuma, Urani, Madini ya Ujenzi na Madini ya Vito.

Amesema pia kuna masoko mawili ya madini ambayo ni Soko la Madini Songea na Soko la Madini Tunduru ambayo yalianzishwa na Serikali kupitia Tume ya Madini ili kuongeza uwazi, usawa, ulinzi wa haki halali na maslahi ya watu wanaofanya biashara hiyo huku akiwataka watanzania kuchangamkia fursa mbalimbali zilizopo mkoani humo kama usambazaji wa teknolojia zinazotumika migodini, usambazaji wa bidhaa za vyakula, uchimbaji, uchenjuaji na biashara ya madini.




 

Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI