Header Ads Widget

TRUMP ALINGANISHA USHURU WA KIMATAIFA NA ATHARI ZA SOKO KAMA ‘KULA DAWA’

 


Saa chache kabla ya kile ambacho wengine wanatabiri inaweza kuwa soko la kihistoria linalouzwa Jumatatu asubuhi juu ya ushuru wa Marekani, Rais Donald Trump alilinganisha sera zake - na athari – na kula dawa.

"Sitaki chochote kishuke, lakini wakati mwingine lazima ule dawa kurekebisha kitu," Trump alisema kwa waandishi wa habari kwenye ndege ya Rais Air Force one jumapili.

Akiendelea kugusia matozo ya ushuru ambayo amewekea mataifa mbalimbali ulimwenguni Trump ameendelea kusisitiza ajira na uwekezaji utarejea Marekani.

"Ni nini kitatokea kwa soko, siwezi kukuambia.Lakini nchi yetu ina nguvu zaidi."Trump asema.

Wakati huo huo, Waziri mkuu wa Japan, Shigeru Ishiba amesema serikali yake itazisaidia kampuni zilizoathirika na nyongeza mpya ya ushuru iliyotangazwa na Marekani wiki iliyopita.

Japan ambayo ni msafirishaji mkubwa wa bidhaa zake kuelekea Marekani imesema itachukua pia hatua za kulinda ajira lakini pia itaendelea kutafuta kulegezewa masharti na Marekani.

Hayo yakijiri, Rais Trump anatarajiwa kukutana na Waziri Mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu Jumatatu na wawili hao wana uwezekano wa kujadili asilimia 17 ya ushuru wa Israel waliotozwa na Trump Kwa mujibu wa gazeti la Marekani la Politico.

Netanyahu alisema Jumapili anatarajia kutafuta afueni kutoka kwa Trump juu ya ushuru waliowekewa.

Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI