Sudan Kusini imesikitia uamuzi wa Marekani wa kubatilisha viza zinazomilikiwa na raia wake wanaotaka kuingia Marekani kutokana na mzozo wa uhamiaji licha ya wao kuwa tayari kushirikiana na Washington.
Kwa mujibu wa Wizara ya Mambo ya Kigeni kupitia mtandao wa Facebook mwanamume ambaye walimkataa kumpokea kuingia nchini humo tarehe 6 mwezi huu baada ya kufukuzwa kwa kukosa kibali cha kuishi Marekani alikuwa ni raia wa DRC na sio raia wake kama ilivyosemekana.
‘’Rekodi ambazo wanazo zinaonyesha kuwa Bwana Makula Kintu aliyezaliwa mwaka 1977 mwezi Aprili tarehe 2 ni raia wa Kongo na sio Sudan Kusini,’’ Wizara hiyo ilisema.
"Serikali ya Sudan Kusini inaelezea masikitiko yake kwa hali iliyosababisha hali hii."
Tarehe 5 Aprili, Marekani ilibatilisha viza zote zilizokuwa na wamiliki wa pasipoti wa Sudan Kusini kutokana na "kushindwa" kwa taifa hilo la Afrika "kukubali kurejeshwa kwa raia wake kwa haraka".
Utawala wa Rais wa Amerika Donald Trump umechukua hatua kali za kuimarisha utekelezaji wa sheria za uhamiaji, ikiwa ni pamoja na kuwarejesha makwao watu wanaoaminika kuwa Marekani kinyume cha sheria.
Utawala huo umeonya kwamba nchi zitakazoshindwa kuwapokea raia wao kwa haraka zitachukuliwa hatua, ikiwa ni pamoja na kuwekewa vikwazo vya visa au ushuru wa forodha.
0 Comments