Header Ads Widget

WAZIRI KITILA KUFUNGUA WIKI YA AZAKI ARUSHA

 




Na Pamela Mollel,Arusha 

Waziri wa  mipango na uwekezaji profesa Kitila Mkumbo  anatarajiwa kufungua  maadhmisho ya wiki ya azaki mwaka 2024 itakayoshirikisha  zaidi ya washiriki   mia sita kutoka sekta binafsi,serikali na wadau wa maendeleo itakayofanyika kuanzia tarehe 9 hadi September 13  jijini Arusha.


Akizungumza na waandishi wa habari kutoka vyombo mbalimbali vya habari Mkoani Arusha,Mkurugenzi mkazi wa CBM International na Mwenyekiti wa kamati ya maandalizi ya wiki ya Azaki,Nesia Mahenge anasema watu zaidi ya 600 wanatarajiwa kushiriki pamoja na mashirika zaidi 400 kutoka ndani na nje ya Nchi


Anasema kuwa wiki hiyo  ya azaki inajumuisha Azaki zote za kiraia ambazo zinashughulika katika maendeleo ya nchi ikiwa ni pamoja na kuwepo kwa balozi wa Canada 


Naye , Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Foundation for Civil Society (FCS), Justice Rutenge, anasema wiki hiyo imebebwa na kaulimbiu isemayo; Sauti, Dira na Thamani ikiendana na wakati uliopo na matukio yanayoendelea nchini, ambayo ni ya  uchaguzi wa serikali za mtaa utakaofanyika mwaka huu, uchaguzi mkuu wa mwakani na uandaaji wa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2025-2050.



 Aidha ameongeza kuwa, wiki hiyo pia itakuwa na mijadala mbalimbali inayohusu shughuli za AZAKi nchini, maendeleo ya jamii na ushirikiano baina ya asasi za kiraia, serikali na sekta binafsi.


Maadhimisho ya wiki ya AZAKi 2024 ni ya sita kufanyika tangu kuanzishwa kwake mwaka 2018.


Hata hivyo Zaidi ya  vijana 70 wanatarajiwa kushiriki katika wiki hiyo ambapo watapata fursa ya kuweza kujifunza maswala mbalimbali juu ya ushiriki wao katika demokrasia  na namna wanavyotakiwa  kushiriki katika shughuli za  ujenzi wa Taifa


“ Mahenge .

ameongeza kuwa ,kupitia maadhimisho  hayo ambayo kufanyika kila mwaka yameleta mafanikio makubwa sana kutokana na wananchi kuweza kujifunza maswala mbalimbali kutoka kwa wengine

"

Kwa upande wake Mkuu wa kitengo cha sekta za umma kutoka benki ya Stanbic  , Doreen Dominic  amesema kuwa,wamekuwa wakifanya wiki hiyo kwa mfululizo  mwaka wa  sita  sasa huku lengo kubwa likiwa ni kupaza sauti ya pamoja katika maswala mbalimbali .

Ameongeza kuwa,kupitia wiki hiyo  wanaungana na taasisi mbalimbali katika  kufanya maboresho mbalimbali na kujadili sauti ya pamoja na kuhakikisha wanapigania haki za watanzania wote waliopo katika maeneo mbalimbali ili waweze kupata haki zao za msingi .



Mkurugenzi wa Haki elimu ,John Kalaghe   amesema kuwa kupitia wiki hiyo kutakuwepo na kipindi   cha vijana ambapo wataweza kushiriki kikamilifu na kujadili juu ya ushiriki wao katika kuandaa majadiliano kwa vijana  juu ya nafasi zao na ushiriki wao katika nafasi mbalimbali. 


Mkurugenzi wa Mtandao wa jinsia Tanzania Tanzania (TGNP),Lilian Liundi amesema kuwa,zaidi  ya waandaaji 20 kutoka asasi za kiraia wakishirikiana katika kuandaa wiki  hiyo ambapo kauli mbiu ya mwaka huu ni sauti,dira na dhamani. 


"Zaidi tunataka sauti za wananchi iweze kusikika

Kwa kuwa kuna umuhimu mkubwa wa kuweka sauti za wadau wote"anasema Liundi

Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI