Na Matukio daima App,
Rais wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan amemuagiza Waziri wa Maji, Jumaa Aweso na Timu yake, wahakikishe ndani ya miezi mitatu maji yanatoka eneo la Mtyangimbole Mkoani Ruvuma.
Rais Samia ameagiza hayo wakati akiweka jiwe la msingi katika Mradi wa Maji Mtyangimbole leo ikiwa ni muendelezo wa ziara yake ya kukagumia miradi ya maendelea, kuzindua na kuwekea mawe ya msingi mkoani Ruvuma.
“Ninawapa miezi mitatu tu, siku 60 za kazi na mwezi mmoja kufanya yale ambayo mmechelewa, mwezi wa 12 Christmass ikiingia maji yawe mwaa..mwaa..mwaa”
0 Comments