TAARIFA KWA UMMA
Kampuni ya Honora Tanzania Public Limited ("TIGO") inatambua taarifa za hivi karibuni kwenye vyombo vya habari kuhusu kesi inayoendelea ya ajira katika mahakama ya ajira ya London inayomuhusisha mfanyakazi wa zamani wa Millicom, kampuni mama ya Tigo hadi mwaka 2022.
Kampuni ya sasa mama ya Tigo haikuwa mmiliki wa Tigo wakati tukio hilo lilipotokea.
Ingawa hatuwezi kutoa maoni juu ya undani wa kesi hiyo, kwani hatuhusiki katika shauri hilo, tunapenda kuwahakikishia wateja wetu na wadau wetu kwamba kulinda taarifa zao binafsi kwa mujibu wa sheria na kanuni za Jamhuri ya Muungano wa Tanzania bado ni kipaumbele chetu cha juu zaidi.
1 Comments
This comment has been removed by the author.
ReplyDelete