Header Ads Widget

TET NA EDUCATE WAINGIA MAKUBALIANO

 



Na Matuko Daima Media, Dar es Salaam

Taasisi ya Elimu Tanzania (TET) na Educate! leo Julai 8, 2024 wameingia makubaliano ya kushirikiana kwa miaka sita katika utekelezaji wa mtaala ulioboreshwa ikiwamo katika somo jipya la Elimu ya Biashara  ambalo ni la lazima kuanzia  kidato cha kwanza hadi cha nne.

 

Katika hafla ya makubaliano hayo, Mkurugenzi Mkuu wa TET, Dk. Aneth Komba  amesema kuwa , makubalino hayo yamekuja wakati muafaka na  kwamba somo la  Elimu ya Biashara litawasaidia wanafunzi nchini kujiajiri mara baada ya kuhitimu masomo yao.

 


“Tunashukuru wenzetu wa Educate! kwa kuendelea kushirikiana nasi  katika kuhakikisha somo la Elimu ya Biashara linafundishwa katika viwango vya juu wakati huu wa kutekeleza Mtaala ulioboreshwa”amesema.

 

Dk. Komba ametaja maeneo kadhaa waliyokubaliana  kushirikiana  na Educate! ni kutoa mafunzo  kwa walimu kazini wa somo la Elimu ya Biashara  katika kutekeleza mtaala ulioboreshwa, kuajiri walimu wa Elimu ya Biashara kwa mkataba katika shule za sekondari ambazo zitakuwa na uhaba wa walimu wa masomo hayo, na maeneo mengine.

 


Kwa upande wake ,Mkurugenzi Mkaazi wa Mahusiano wa Educate!, Kamanda Kamiri amesema kuwa wao wataendelea kushirikiana na TET katika kuhakikisha  somo la Elimu ya Biashara nchini linafundishwa na kueleweka kwa wanafunzi ambao wanatarajiwa kufanya vyema katika eneo la ujasiriamali.

 

“Ni jambo jema kwetu kuendelea kushirikiana na  TET katika eneo la ufundishaji na ujifunzaji wa somo la Elimu ya Biashara kwa wanafunzi wa Tanzania" amesema  Kamiri.



Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI