MKUU wa Mkoa Pwani Abubakar Kunenge ameipongeza Halmashauri ya Mji Kibaha kwa kutobweteka kwa hati safi kutoka kwa Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) bali iongeze ukusanyaji mapato.
Akizungumza kwenye kikao cha Baraza la Madiwani wa Halmashauri ya Mji Kibaha kilichofanyika Kibaha wakati wa kupitia hoja za CAG.
Kunenge amesema kuwa Halmashauri imefanya vema kwa ukusanyaji wa mapato kutoka asilimia 54 Februari na kufikia asilimia zaidi 100 ambapo ni kazi kubwa imefanyika.
"Nawapongeza kwa kazi kubwa mliyoifanya lakini mnapaswa kudhibiti matumizi ya fedha kwani baadhi ya hoja zimetokana matumizi ya fedha na kutekeleza miradi kwa wakati,"amesema Kunenge.
Kwa upande wake katibu wa baraza hilo ambaye ni Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji Kibaha Dk Rogers Shemwelekwa amesema kuwa kulikuwa na jumla ya hoja 69 zikiwemo za nyuma ambapo hoja 31 zimefungwa.
Kwa upande wake Mwenyekiti wa Halmashauri ya Mji Kibaha Mussa Ndomba amesema kuwa wanaomba bajeti ya barabara iangaliwe kwani miundombinu imeharibika sana.
Ndomba amesema kuwa Halmashauri hiyo ipewe msukumo wa kuwa Manispaa kwani hapo ni Makao Makuu ya Mkoa huo kwani hata baadhi ya miradi inaweza kupatikana.
Naye Mkaguzi wa Mkuu wa nje wa Mkoa wa Owabi Pastory Massawe amesema kuwa baadhi ya changamoto zimeonekana kwenye eneo la ukusanyaji wa mapato.
0 Comments