NA THABIT MADAI, ZANZIBAR -MATUKIO DAIMA
RIPOTI ya Mpya ya masuala ya Fedha (Finscope) Tanzania 2023 ripoti mahususi ya Pili ya Zanzibar imezinduliwa rasmi na Makamu wa Pili wa Rais Hemed Suleiman Abdulla kwa niaba ya Rais wa Zanzibar Dk.Hussein Ali Mwinyi ambayo inaonesha Mahitaji, matumizi na upatikanaji wa huduma jumuishi za fedha yameongezeka kutoka Asilimia 45 mwaka 2017 hadi asilimia 82 mwaka 2023.
Aidha ripoti hiyo inaonesha kuwa, Zanzibar ina idadi kubwa ya watu wanaoweka akiba ya Fedha huku Matumizi ya Bima yakiwa madogo ukilinganisha na maeneo mengine Tanzania.
Hata hivyo ripoti hiyo inaonesha kiwango cha utegemezi kwa watu bado kipo juu Visiwani Zanzibar.
Akihutubia Wananchi mara baada ya uzinduzi wa ripoti hiyo, Makamu wa Pili wa Rais amesema kuwa, Serikali inaridhishwa na matokeo ya utafiti huo ambao unaonesha hali ya matumuzi jumuishi ya huduma za fedha yameongezeka kwa asilia 82 mwaka 2023 kutoka 45 mwaka 2017.
Amesema kuwa, Tahiti zinaonesha uwiano wa ujumuishaji wa fedha kwa jinsia zote umepungua kwa asiliamia kubwa huku uchumi wa Wanawake ukiongeza na kuondokana na utegemezi.
Aidha kulingana Mafanikio ya utafiti huo Serikali imejipanga kuhakikisha kuwa maendeleo ya sekta ya fedha ba huduma za fedha jumuishi zinaimarika zaidi.
Amesema, sote ni mashahidi wa namna ambavyo matokeo ya Utafiti wa Finscope Tanzania 2017 ripoti ya Zanzibar, yalivyosaidia michakato mbalimbali ya kuboresha na kuongeza upatikanaji wa bidhaa na huduma jumuishi za fedha kwa wananchi.
"FinScope imesaidia watunga sera kufanya mapitio ya sera kikamilifu, kuunda zana za ufuatiliaji kwenye sekta ya fedha, na kuweka mikakati ya kuongeza ustawi na huduma jumuishi za fedha. Kwa wadau wa sekta binafsi, FinScope imewasaidia kubuni bidhaa na huduma za fedha zinazoendana na soko na kukidhi mahitaji ya wateja."
Mapema Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Fedha na Mipango Zanzibar Sada Mkuya amesema kuwa utafiti huo ni njezo muhimu inayoweza kutumika na wadau wote kama Dira ya kufanya maamuzi sahihi kwa maendeleo ya nchi.
"Utafiti huu tutauchukua na kuufanyia kazi kwa kuusambaza kwa wadau wote ili wachukue hatua stahiki," ameeleza.
Ameeleza kuwa utafiti huo unasaidia kubuni bidhaa za fedha zinazoendana na soko na kukidhi mahitaji ya wateja
Utafiti huo hupima mahitaji, upatikanaji na matumizi ya huduma zafedha Unguja na Pemba.
0 Comments