Header Ads Widget

GAVANA WA BENKI KUU AHIMIZA HOTELI KUTOA HUDUMA ZA KUBADILISHA FEDHA

 Na Mwandishi Wetu.

GAVANA wa Benki Kuu ya Tanzania (BOT) Emmanuel Tutuba amewahimiza wamiliki na waendeshaji wa Hoteli zenye hadhi  ya nyota Tatu hadi Tano Zanzibar kuchangamkia fursa ya kupata leseni  na  kuanza kutoa huduma za kubadilisha fedha za kigeni ili kupunguza soko haramu  la ubadilishwaji wa fedha.

Wito  huo  ameutoa leo  katika mkutano na baadhi ya Wamiliki na waendeshaji  wa Hoteli zinazopokea watalii nchini uliofanyika katika Ofisi ndogo za Makao Makuu ya Benki Kuu Gulioni Zanzibar ambapo  amesema kuwa, kutokana  na Mabadiliko ya Sheria  inatoa fursa kwa Hoteli kutoa huduma za kubadilisha fedha jambo ambalo linasaidia kuondoa usumbufu  kwa wateja wao.

Aidha Gavana ameeleza kuwa msingi wa kufanya  marekebisho ya Kanuni umetokana na utafiti uliofanywa na Benki Kuu na kugundua urasismishwaji wa maduka ya fedha za kigeni haukuhusisha hoteli na kuchochea soko kubwa la biashara haramu za kubadilisha fedha za kigeni.

Mkutano huo uliohudhuriwa na wamiliki na waendeshaji wa Hoteli unatokana na hatua iliyochukuliwa na Benki Kuu ya kurekebisha kanuni ya maduka ya kubadilisha fedha za kigeni ambapo Sheria hiyo inaruhusu hoteli za kitalii kupata leseni za kutoa huduma za kubadilisha  fedha za kigeni kwa wateja wao.


Post a Comment

0 Comments



MAGAZETI



NAMBA ZA HUDUMA YA USAFIRI WA KUKODI